Skip to main content

Posts

Showing posts from March 2, 2016

WAZIRI UMMY MWALIMU APOKEA MSAADA WA FEDHA WA MIL 220, KWA MATIBABU YA WAGONJWA WA MOYO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Ally Mwalimu leo Machi 2.2016, amepokea msaada wa fedha kwa ajili ya kuwezesha matibabu ya wagonjwa wa moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo kwa msaada huo, jumla ya watoto 101, wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo katika taasisi hiyo kwa gharama za fedha hizo zilizotolewa na Jumuiya ya Kihindu waishio Dar es Salaam ijulikanayo kama BAPS Charity, kwa kuguswa kwao na kutoa msaada mkubwa na upendo waliouonyesha kwa watanzania wanaosumbuliwa na maradhi ya moyo. Wiziri Ummy amebainisha kuwa, kiasi cha msaada unaotolewa utawezesha wagonjwa wapato hao kupatiwa matibabu ya moyo hivyo kuwa, faraja kubwa kwa wagonjwa waliokuwa wakisubiria huduma hizo kwa muda mrefu kutokana na kushindwa gharama za matibabu yake. Aidha, kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Mohamed Janabi amepongeza kwa msaada hu...

MAGAZETINI LEO ALHAMISI

MAMLAKA YA HALI YA HEWA NCHINI TMA, YAWAPIGA MSASA WANAHABARI KUHUSU EL-NINO NA ATHARI ZAKE

Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Marcella Mayalla, akifungua Warsha ya Siku mbili kwa Wanahabari Kuhusu El-Nino na athari zake katika Mvua hapa nchini, iliyofanyika hii leo Jijini Mwanza.  Mayalla amefungua Warsha hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo. Na:George Binagi-GB Pazzo Katika Warsha hiyo, Taasisi mbalimbali pamoja na Wanajamii, zimehimizwa kutumia taarifa za Utabiri wa Hali ya Hewa kwa ajili ya Mipango ya Maendeleo. Pia Wanahabari ambao ni kiunganishi Muhimu katika upashanaji wa habari, wametakiwa kutumia nafasi yao katika kutoa taarifa hizo kwa wananchi ikizingatiwa kwamba, taarifa za utabiri wa hali ya hewa zikiwafikia walengwa kwa wakati, husaidia kujikinga na maafa yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo Mafuriko na ukame. Warsha hiyo imeandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Hali ya Hewa Duniani (WMO) ikiwa ni katika mpango wake wa Kidunia katika kuboresha upati...