Skip to main content

Posts

Showing posts from February 16, 2026

Mradi wa Maji Warejesha Tabasamu kwa Wanafunzi wa Jamhuri

  Mbarali. Wanafunzi wa Shule ya Msingi Jamhuri iliyopo Kijiji cha Ilongo, Kata ya Ilongo wilayani Mbarali mkoani Mbeya, wameanza kunufaika na mradi wa maji safi uliotekelezwa na Rufiji Basin Water Board kupitia Mradi wa NBS-USANGU. Kabla ya utekelezaji wa mradi huo, wanafunzi walilazimika kutembea zaidi ya kilometa tatu kutafuta maji, hali iliyokuwa ikiathiri mahudhurio yao, kuongeza uchovu na kuchelewesha masomo. Wengine walilazimika kufika shuleni wakiwa wamechoka, jambo lililopunguza umakini darasani. Kupitia mradi huo, kisima kirefu kimechimbwa na maji kusambazwa moja kwa moja shuleni pamoja na kwa wananchi wa maeneo jirani, hatua iliyoboresh­a mazingira ya kujifunzia na kuimarisha usalama wa wanafunzi. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi hivi karibuni , Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Jenifer Sanga, alisema upatikanaji wa maji ndani ya shule ni mabadiliko makubwa kwa ustawi wa wanafunzi. “Hii ni faraja kubwa kwetu. Sasa wanafunzi hawatapoteza muda kutafuta maji na watawe...