KILOLO: WANANCHI wa kijiji cha Mawala, kata ya Irole katika Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wameitaka serikali wilayani humo kuharakisha upimaji wa maeneo ya ardhi ya kijiji chao pamoja kupatiwa cheti cha ardhi ya kijiji ili kupunguza migororo mbalimbali iliyopo kwa sasa. Wakizungumuza jana katika mdahalo walisema serikali kwa kutumia sheria ya ardhi ya vijiji itenge maeneo kwa ajili ya wakulima na wafugaji hatua itakayosaidia makundi hayo kuepukana na migogoro kwa kuwa makundi yote mawili yanategemeana. Mdahalo huo uliozungumzia namna ya kuondoa migogoro ya ardhi ya kijiji uliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Grassroots Oriented Development (TAGRODE) yenye makao yake makuu mjini Iringa kwa shirikiana na PELUM Tanzania . Wakichangia mada, wakazi hao wa Kijiji cha Mawala walisema migogoro ya ardhi katika maeneo yao itakoma kama serikali itasimamia kwa nguvu zake zote utekelezaji...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.