Skip to main content

MBUNGE WA MUFINDI KASKAZINI ATINGA KORTINI TENA LEO

KESI ya kutoa hongo katika mchakato wa kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) inayomkabili aliyekuwa Mbunge wa Mufindi Kaskazini na Waziri katika serikali za awamu zote nne, Joseph Mungai imetajwa tena leo (Agosti 25) katika Mahakama ya Mkoa wa Iringa.
Mungai (66) pamoja na makada wengine wawili ambao ni Katibu wa Umoja wa vijana wa CCM wa Wilaya ya Mufindi, Fidel Cholela (39) na Moses Masasi wanakabiliwa na mashtaka 15 ya rushwa kinyume na sheria ya kuzuia na kupamna na rushwa ya mwaka 2007 na sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 .
Watuhumiwa hao kwa pamoja, kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Agosti 11, mwaka huu na kusomewa mashitaka hayo ambayo pia waliyakana.


Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkoa, Marry Senapee, ambapo upande wa mashitaka uliokuwa ukiongozwa na Prisca Mpeka kutoka Takukuru, uliomba tarehe nyingine ya shauri hilo kwa ajili ya kusoma maelezo ya awali yanayoweza kuruhusu kuanza kusikiliza kesi hiyo.


Hata hivyo, Wakili anayewatetea washitakiwa hao, Basil Mkwatta aliomba tarehe itakayopangwa na mahakama hiyo alete pingimizi la awali la kisheria kwamba kesi hiyo haistahili kuwepo mahakamani hapo.


Pande zote mbili zilikubaliana ambapo Hakimu Senapee alipanga kesi hiyo irejeshwe mahakamani hapo Septemba 30 mwaka huu ambapo Mkwatta ataleta pingamizi hilo na hivyo kumfanya mwendesha mashitaka wa Takukuru,Prisca Mpeka asisome maelezo ya awali siku hiyo na badala yake atalazimika kusubiri kusikia pingamizi hilo na kutoa hoja za kujibu.


Inadaiwa kuwa Julai 08, mwaka huu, katika kata ya Ihalimba, Wilaya ya Mufindi, Mungai akiwa mmoja wa makada wa CCM waliokuwa wanawania kupitishwa katika kura za maoni kugombea ubunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, kwa pamoja na watuhumiwa wenzake, walitoa hongo ya Sh.10,000 kwa Mwenyekiti wa CCM tawi la Vikula kama kishawishi cha kumpigia kura wakati wa zoezi la upigaji wa kura za maoni.


Katika shtaka la pili, inadaiwa kuwa watuhumiwa wote kwa pamoja, siku na katika eneo hilo walitoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Konjesta Kiyeyeu ambaye alihudhuria kikao cha kamati ya CCM Kijiji cha Vikula.


Mwendesha mashitaka huyo aliendelea kudai mahakamani hapo kuwa, katika shtaka la tatu, nne, tano na sita, watuhumiwa wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Aldo Lugusi, Ezekiel Mhewa, Tulaigwa Kisinda na Jiston Mhagama kwa lengo hilo hilo la kuwashawishi wampigie kura za maoni.


Katika shitaka la saba,watuhumiwa hao wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.20,000/- kwa Maria Kihongosi na shtaka la nane kutoa hongo ya Sh.5,000/- kwa Lurent Mdalingwa wakati shtaka la tisa wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.20,000/- kwa Victory Kalinga ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Kijiji cha Ugessa.


Katika mashtaka namba kumi hadi 12 washtakiwa wote kwa pamoja wanadaiwa walitoa hongo ya Sh.2,000/- kwa Francis Chonya, Alfred Kisinga na Issac Tewele wakati shtaka la 13 wanadaiwa walitoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Sosten Kigahe.


Aidha, Mwendesha mashitaka huyo alidai kuwa shitaka namba 14 watuhumiwa wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Raphael Lutumo na shitaka la mwisho walitoa hongo ya Sh.20,000/- kwa Andrew Mkiwa.


Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...