Skip to main content

MTIHANI KIDATO CHA SITA: WASICHANA MAPOSENI KUWAONYESHA KAZI WAVULANA

 Sehemu ya wahitimu 53 wa Shule ya Sekondari ya Maposeni wa Kidato cha Sita wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kuanza sherehe ya Mahafali ya Pili 2011.

Mkuu wa Shule ya Maposeni Sekondari, Humari Mapunda akisoma taarifa ya maendeleo ya shule kwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya Pili ya kidato cha Sita 2011. 

BAADA ya wasichana kung’ara Kidato cha Nne 2010, nao wasichana wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Maposeni wamenena kuwaonyesha kazi wavulana katika mtihani ya Kidato cha Sita Mwaka 2011.


Hivi karibuni Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) lilitangaza matokeo ya mtihani wa Kidato cha Nne uliyofanyika Oktoba mwaka jana yaliyoonyesha kuwa wasichana waliongoza kwa kiwango cha ufaulu.


Hata hivyo, matokeo hayo yameonyesha kuwa kiwango cha ufaulu katika mtihani huo kimeshuka kwa asilimia 22 ikiliganishwa na matokeo ya mwaka 2009 kuwa wasichana walifanya vizuri zaidi kuliko wavulana, alisema Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk Joyce Ndalichako.


Wasichana hao wa Shule ya Sekondari ya Maposeni walisema hayo Ijumaa wiki jana katika Mahafali ya Pili ya Kidato cha Sita Mwaka 2011 yaliyofanyika Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma.


Baadhi ya wasichana waliongea na Nipashe ni Waridi Hyera na Selesia Kinundu walisema kuwa kama wasichana waliowatangulia walivyofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita mwaka jana nao pia watafuata nyayo kwa kufanya vizuri zaidi katika mtihani wao utakaofanyika tarehe 7. 2. 2011.


Historia inaonyesha kuwa shule hiyo wasichana 50 wa mara ya kwanza walifanya vizuri katika mtihani ya kidato cha sita 2010. Hivyo basi mwaka 2010 walifanya mahafali ya kwanza ya kidato cha sita na walikuwa ni wasichana tu.


Shule huyo ilianza kuwa na Advanced level April 2008, kwa hiyo wahitimu wa kwanza wa kidato cha sita walimaliza Februari 2010. Machaguo ya masomo wanayosoma hapa ni HGK na HKL. Wahitimu 50 wote walikuwa wasichana, matokeo yao yalikuwa mazuri sana kwani walipata daraja la I, II na III hivyo hakuna aliyepata daraja la IV na 0 mwaka jana.


Wahitimu wa mwaka huu ni 53 wa kidato cha sita kati ya wanafunzi 60 tulioanza kozi hiyo mwaka 2009, kwa sasa waluvana 35 na wasichana 18 nakufanya idadi ya wanafunzi kuwa 53.


Shule hii pia ina wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi nne ambao jumla yao ni 752. Kidato cha tano wapo 69 jumla 821 ya wanafunzi wote.


Katika risala ya wahitimu hao wa kidato cha sita mwaka 2011 kwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili, ilieleza kuwa wanafunzi walianza kidato cha tano wakiwa 60 ambapo wavulana walikuwa 38 na wasichana 22, upungufu huo umetokana na sababu zisizozuilika za kuhama,kutokana sababu za kiafya wanafunzi saba wasiweze kuhitimu ambao wavulana ni watatu na wansichana ni wanne.


Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la PADI, Iskaka Msigwa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo aliwaasa wahitimu kushika huyu elimu kamwe wasichanganye mambo kwani ukimwi utawamaliza kabla hajamaliza elimu ya chuo endapo watafanikiwa kuchaguliwa kujiunga na elimu ya juu mwakani.


“Itakuwa ni kazi bure kwa wazazi au walezi wenu kuwaona mnakufa na ukimwi baada ya kumaliza masomo ya elimu ya juu pia serikali itakosa wataalamu baadae kwa sababu haiwezi kuwaajili watu walioathirika kwa ukimwi…. Kwa hiyo jihadhalini na ugonjwa wa ukimwi unaua” alisema.


Mkuu wa Shule hiyo Humari Mapunda katika taarifa yake aliyoisoma kwa mgeni rasmi alisema kuwa majukumu ya shule ni kutoa elimu ili kufanikisha malengo ya taifa, wanakumbana na vikwanzo mabalimabli, ikiwa ni pamoja na upungufu wa walimu katika masomo ya sanyansi kwa kidato cha 1-4 na mwalimu wa kiingereza kwa kidato cha 5-6, uchakavu wa majengo, ukosefu wa umeme kwa sasa wanatumia umeme wa jenereta ambalo huwashwa kwa msimu hususani vipindi vile vya mitihani.


Matatizo mengine ni ukosefu wa chanzo cha maji ya uhakika, ukosefu wa ukumbi wa chakula na upungufu wa matundu ya vyoo na upungufu ni 18, yaliyopo ni 24 wavulana 11 na wasichana 13, ukosefu wa majengo mawili ya maabara (physics na chemistry), upungufu wa nyumba za walimu zilizopo ni tano upungufu ni 25 (pia nyumba 3 hazijakamilika) na upungufu wa watumishi wasio walimu kama Boharia na Mhasibu.








Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...