Skip to main content

MWENYEKITI TLP SONGEA AFARIKI DUNIA


Na Friday Simbaya,
S ongea
PAROKO Padre Joseph Ndimbo wa Parokia ya Peramiho Jimbo Kuu la Songea aliwaasa  waombolezaji kuacha mara moja tabia kugombeana maeneo ya kuzika marehemu.
Alisema kuwa kuna mtindo umezuka wanandugu kuvutana wapi wamzike marehemu na kuongeza kuwa huku ni kumdhalilisha marehemu.
Pd. Ndimbo alisema hayo Jumamosi wakati wa mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa Tanzania labour Party (TLP)wilaya ya Songea, Bw. Kalo Kombe katika makaburi ya Liangano karibu na Kijiji cha Lipinyapinya Kata ya Peramiho.
Alisema kuwa sio tabia nzuri kwa wanandugu kugombeana maiti , kumbe maeneo yote yanafaa kuzikia.
“Imezuka tabia katika jamii ya watu kugombania maiti yaani mvutanao wa watu wawili kugombania maiti wakati wa  mazishi kila mtu anataka kuzika mahali pake, huku kote ni kuhangaika na kumtesa marehemu. Kuzikwa ni kuzikwa tu hata kama atazikwa Peramiho ‘A’ au Peramiho ‘B’,” alitoa mfano paroko huyu.
Aidha, paroko alisisitiza kuwa watu wasitafute mchawi kwamba marehemu amerogwa bali waendelee kumuonbea marehemu kuwa astarehe kwa amani kwa Mungu Baba.
Aliwaambia waombolezaji kuwa kuumwa kwa mwanadamu ni mateso kwa sababu mtu yeyote atakayependa maisha lazima afe lakini anayechukia maisha ataishi maisha ya milele.
Aliongeza kuwa WaTanzania vilevile tunakiwa  kufanya kazi kwa bidii sio kutafuta kwa njia ya mkato. Alisema kuwa mtu lazima apate mateso ili afe kama vile mtu anatakiwa kuteseka ili apate chakula. Aliongeza kuwa mateso ni sehemu ya maisha ya binadamu, kwa hiyo mtu akiuugua ni mateso, vilevile mtu kuchapakazi kwa bidii ni mateso pia ili kuweza kuishi maisha bora.
“Hakuna maisha bora kama hujishughulishi kwa sababu maisha bora huja kwa kufanyakazi kwa bidii na kuaacha uvivu,” alisema paroko. “Asiyefanya kazi na asile huo ndio wito wangu kwenu” alisisitiza.
Mwenyekiti huyo wa TLP  alifariki dunia juzi katika hospitali ya Misioni ya St. Joseph Peramiho baada ya kuugua vidonda vya tumbo kwa muda mrefu.
Marehemu Kombe alistaafu katika Jeshi la Polisi tangu 1995, ambapo alifikia renki ya inspector kabla ya kustaafu na kuanza kujishughulisha na mambo ya siasa. Marehemu Kombe alipenda magauzi ndiyo maana alijiunga na upinzani, alikuwa anaishi maeneo ya Mjimwema katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...