Skip to main content

WANANCHI WENYE HASIRA LUGARAWA WAKATA MABOMBA YA MAJI YA PAROKO, NI BAADA YA MWENYEKITI WAO KUMPIGIA MAGOTI BILA MAFANIKIO.


LUDEWA

WANANCHI na watumiaji wa maji katika Kitongoji cha Luafyo Juu Lugarawa wilayani Ludewa jana walijawa jazba na kuamua kuyakata kwa mapanga mabomba ya maji yanayotumika pia na Kanisa Katoliki kwa madai kuwa Paroko wao amewanyima maji bila sababu.
Awali August 23 na 24 mwaka huu Mwenyekiti wa Kijiji cha Lugarawa Bw. Erasto Mhagama akiwa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Luafyo Juu walikwenda kumpigia magoti Padri Jordan Mwajombe ili afute msimamo wake na badala yake atoe maji kwa wananchi, lakini alikataa kabisa na kuwafokea kama watoto wadogo viongozi hao.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Luafyo Juu Mzee Thadei Exavery Mwinuka (70) kwa upande wake alisema anayo miaka zaidi ya thelathini katika eneo hilo na muda wote wananchi wake wamekuwa wakitumia maji hayo yaliyoletwa kwa ushikiano wa wenyeji na wamisionari wazungu.
Mzee Mwinuka alisema sababu za wananchi kukata mabomba haya ni kunatokana na ukatili wa Paroko wa Parokia ya Lugarawa Padri Jordan Mwajombe kuwakatia wananchi maji bila kuwasiliana nao huku akitumia ukali kila anapofuatwa kutoa maji. Hata hivyo alimtaka na kumsisitizia Paroko kufungua maji yatumike na wananchi wote kama zamani.
Baadhi ya wananchi waliokutwa katika eneo yalipokatwa mabomba hayo Bathlomeo Mgina, John Haule (75), Benjamin Chengula, Pangista Mtweve na Vestina Mtweve walisema wanalazimika kuchota maji yasiyosalama mtoni kwa sababu Paroko amefunga maji na kwamba asipofungua maji mgogoro utakua mkubwa sana.
Aidha, wananchi hao walimrushia lawama Paroko na mafundi wake waliotajwa kwa jina mmoja mmoja kama John na Mligo ambao amewagawia maji kwa manufaa binafsi bila mawasiliano na kwamba Paroko huyo amekuwa mkali kila anapofuatwa na viongozi.
Awali, akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi  kutaka kujua kiini cha tatizo Pd. Jordani Mwajombe kwa upande wake alisema hajawahi kumwona mtu yeyote akienda kwake kuomba maji na kwamba huo ni unafiki wa watu na hakutaka kutoa maelezo zaidi.
Erasto Mhagama ni Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Lugarawa alisema ameenda kwa Paroko mara kadha na kuamua kumpigia magoti mwenyewe, ili awape wananchi maji wananchi kumaliza mgogoro, lakini ilishindikana kutokana na kauli za ukali anazotumia mchunga kondoo huyo.
Bw. Mhagama alitoa wito kwa mchungaji huyo wa kiroho kuacha ubabe badala yake akubali kukaa na wananchi ili kumaliza mgogoro. Akaongeza kuwa “Kama Paroko atakataa kukaa na wananchi siku ya Ijumaa August 26 na kufanya makubaliano mimi sitajihusisha na sakata hilo tena,” alisema Mhagama.
Hata hivyo, baada ya wananchi hao kumbana na kuonesha msimamo wao Pd. Mwajombe alikubali kuhudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika August 26 katika Kitongoji cha Luafyo Juu alipobanwa na kuambiwa ukweli na akasalimu amri na kuahidi kutoa maji kwa wanakijiji hao.
Chanzo cha maji hayo ni Idokonya ambako ndiko shambani kwa mwenyekiti wa kitongoji cha Luafyo Juu na kwamba wananchi wake walishiriki kwa kuchimba mtaro na wazungu walipokuwa wakijenga Mission ya Lugarawa.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...