Skip to main content

Mratibu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) : PUNGUZENI KASI YA MAAMBUKIZI

SONGEA



Mratibu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Mkoa wa Ruvuma Bwana
Emmanuel Petro amesema kuwa ili kupunguza kasi ya maambukizo ya Virusi
Vya Ukimwi mkoani hapa halmashauri na wadau wengine wa Ukimwi hazina
budi kufanya kazi kwa pamoja.



Alisema kuwa ili kufanikisha mkakati wa taifa wa kinga dhidi ya VVU
halmashauri na wadau wengine wanapaswa kufanya kazi kwa karibu na
hatimaye kuweza kupunguza maambukizo haya.



Mratibu TACAIDS (M) huyo alitoa rai jana katika kikao cha kupitia
mipango ya shughuli za Ukimwi za Halmashauri kilichofanyika Peramiho
kikihusisha Waratibu wa Ukimwi Kinga Wilaya (CHAC) na Waratibu wa
Ukimwi-Tiba katika ngazi ya wilaya yaani (DACC) wa kutoka Halmashauri
zote za Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma yaani Songea Manispaa, Songea
Vijijini, Namtumbo, Mbinga na Tunduru.



Alisema kuwa  lengo la kikao hicho cha siku mbili ni kupima shughuli
za Ukimwi za halmashauri  kama zinaendana na miongozo ya kitaifa,kama vile
vile Mkakati wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi-2009-2012 na Mkakati wa
Taifa wa Kinga ya Virusi Vya Ukimwi.



“Mkakati wa Taifa wa Kinga ya VVU unaweka fursa na mwongozo wa
kuongeza maradufu juhudi za taifa za kuzuia idadi ya maambukizo ya
VVU. Dira inatokana na ile ya mkakati wa taifa wa kudhibiti
UKIMWI-Tanzania bila ya maambukizo ya VVU- kwa kupunguza kiwango na
idadi ya mambukizo ya VVU kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2012. Mkakati
huu ni matokeo ya ushirikiano wa sekta ya umma, binafsi na vyama vya
kiraia, kwa kuidhinishwa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS),” kwa
mujibu wa taarifa kutoka TACAIDS.



Bw. Petro aliongeza kuwa lengo la hatua zote hizo ni kuhakikisha
kwamba harakati za mapambano dhidi ya vvu na ukimwi zinaendeshwa kwa
kuzingatia miongozo ya serikali kwa kuwashirikisha wadau wote na
wananchi kwa ujumla, kwa kupitia utaratibu wa uandaaji wa mipango
shirikishi jamii kwa mfumo wa fursa na vikwazo kwa maendeleo ambayo
ndio dhana ya kuishirikisha jamii katika kushiriki kikamilifu katika
kuibuia matatizo na fursa zilizopo katika kuwa na mipango mizuri
katika kudhimbiti UKIMWI katika mkoa wetu.



“Janga la UKIMWI limedhihirika kugusa sekta zote za jamii na hivyo
kuwa suala mtambuka katika shughuli zote za kiuchumi, kijamii na
kiutamaduni.”



Lakini pia Mratibu huyu ameziagiza halmashauri pamoja na wadau wengine
wanaoshuhulikia masuala ya Ukimwi zitenge fedha katika bajeti zao za
kwa ajili ya masuala ya Ukimwi  badala ya kutegemea wafadhili peke yao
ambapo kwa kufanya hivi watakuwa wamepunguza kasi ya maambukizo mapya
ya ugonjwa huu.



Katika kufanikisha azma wananchi na viongozi wanapaswa kuwa mstari wa
mbele katika kujitokeza katika vituo mbalimbali vya kupima na kupokea
ushauri nasaha ili kuweza kujua afya zao na hatimaye kupanga mikakati
stahiki ya maisha yao, ambapo kwa wote wanaokutwa na Virusi vya Ukimwi
Serikali inatoa bure dawa ya kurefusha na kupunguza makali ya virusi
vya Ukimwi (ARVs) katika vituo vya kutolea huduma hiyo.



Mkoa wa Ruvuma una maambukizi ya virusi vya Ukimwi asilimia 5.8%
wakati kitaifa ni 5.7% ambapo kasi ya maambukizi ya ugonjwa huu kimkoa
inazidi ile ya Taifa kwa asilimia 0.1%  kutokana na utafiti wa
viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria ya kitaifa uliyofanyika mwaka
2007/2008 (THIS).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...