Skip to main content

KIWANDA CHA PERAMIHO PRINTING PRESS CHA PATA PIGO


Na Friday Simbaya, Songea
Mamia ya wakazi wa Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma wamzika mfanyakazi wa kiwanda cha uchapishaji cha Peramiho (Peramiho Printing Press), Mzee Bernhard Mhagama (55) katika makaburi ya Lundusi leo (Alhamisi).

Mzee Mhagama ambaye pia alikuwa kiungo kikuu katika Kiwanda cha Uchapishaji cha Peramiho katika masuala ya kompyuta alifariki dunia tarehe 02.04.2013 baada ya kuanguka ghafla wakati wakielekea kijiji cha Lugarawa kwenye msiba wa mama yake mzazi, ambapo hata hivyo hawakuwahi mazishi.

Ibada ya Misa ya mazishi iliongozwa na Padri Benedict OSB ambaye pia ni Paroko msaidizi wa Parokia ya Peramiho kwa kushirikiana na Paroko wa Parokia ya Lugarawa – Njombe, Pd. Jordan Mwajombe.

Akiongea na Nipashe mdogo wa marehemu Beda Mhagama alisema kuwa baada ya kupata taarifa ya misba kwamba mama yao amefariki walifunga safari yeye na marehemu (Mzee Mhagama) pamoja na baadhi ya ndugu, lakini walipofika mjini Njombe kaka yake alizidiwa na kukimbizwa katika hospitali ya Kibena, Njombe na baadaye kupelekwa hospitali ya misheni ya Peramiho kwa matibabu zaidi kutokana na ugonjwa wa BP ya kupanda, ambapo hata hivyo haikuwezekana kuokoa maisha yake.

“Hapo awali marehemu mzee Mhagama alifiwa na baba mkwe wake,( yaani baba mzazi wa mke wake), ambapo msiba ulikuwa nyumbani kwake katika Mtaa wa Lipinyapinya Kata ya Peramiho, Wilaya ya Songea Vijijni mkoani Ruvuma, lakini kesho yake tena marehemu akapata taarifa ya kufiwa na mama yake mzazi huko Lugarawa, ndipo Jumapili tarehe 28.03.2013 tuliondoka na baadhi ya wanafamilia kuelekea Lugarawa kumzika mama yetu ndipo umauti ukamkuta,” alielezea mdogo wa marehemu.
Marehemu Bernhard Mhagama alizaliwa mwaka 1958 huko kijiji cha Lugarawa, Njombe. Alimaliza shule ya msingi mwaka 1974 ambapo baadaye alijiunga na ufundi uwashi huko Uwemba mwaka 1975 – 1976.

Mwaka 1978 alijiunga na Kiwanda cha uchapishaji cha Peramiho (Peramiho Printing Press), mwaka 1980 marehemu alifunga ndoa katika Kanisa la Kitawa la Abasia ya Peramiho. Marehemu ameacha mke na watoto nane (8), wa kiume wanne na wa kike wanne, na wajukuu watano.
Kabla ya kifo chake marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa BP ya kupanda tangu 2000 hadi mauti yalipomfika asubuhi ya tarehe 02.04.2013 katika hospitali ya Mtakatifu Joseph – Peramiho.

Wakati huohuo, mkuu wa kiwanda cha uchapishaji Peramiho Br. Sylvester Ndoga OSB, ambacho kinamilikiwa na Peramiho Benedictine Fathers, alimuelezea marehemu kama mtu aliyefanya kazi kwa moyo wote ambaye hakuwahi kuchelewa kazini, na pia alikuwa na ushirikiano mzuri na wafanyakazi wenzake.

Mwisho












Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...