Skip to main content

SHULE YA PERAMIHO INAONGOZA KIWILAYA

Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Peramiho, Jane Mkuwa. (Picha na Friday Simbaya)


Na Friday Simbaya, Songea
Shule ya Msingi Peramiho, Wilaya  Songea Vijijini mkoani Ruvuma,  imepanda na kushika nafasi ya kwanza kiwilaya kutoka nafasi ya pili mwaka jana kati ya  ya shule 89, imefahamika.
Akiongea  na MWENGE, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Peramiho,  Jane Mkuwa leo ofisini kwake alisema shule yake imepanda nafasi ya kwanza kiwilaya kati ya shule 89 ukilinganisha na mwaka jana ambapo shule hiyo ilishika nafasi ya pili.
Aidha, shule hiyo imekuwa  ya sita kimkoa kati ya shule 719 na nafasi ya 428 kitaifa kati ya jumla ya shule 15,656. Shule hiyo  ina jumla ya walimu 20 wakiwemo  walimu wa kike  kumi na tano na wakiume wa  tano.
Alisema kuwa watahiniwa waliofanya  mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa mwaka 2013  walikuwa 33 na wote  wamefaulu, sawa na asilimia 100 ya ufaulu. Wanafunzi waliopata alama za juu kuliko wengine ni wanafunzi wawili tu, ambao ni Eberhat Selestini Komba na Faraja Elias Katulu waliopata wastani wa daraja la ‘A’.
“Tangu nimekuwa Mwalimu Mkuu katika  shule hii mwaka 2010 nikitokea Shule ya Msingi Mapinduzi, Wilaya ya Songea vijijini, mkoani Ruvuma, shule yangu imekuwa na mafanyikio makubwa. Mafanikio yote haya ni     kutokana na ushirikiano mzuri wa walimu,” alisema mwalimu mkuu.

Aliongeza kuwa mwaka 2010 na 2011 shule hiyo ilikamata nafasi ya nne kwa miaka miwili  mfululizo  kwa ufaulu wa asilimia 66. Mwaka 2012 na 2013 shule hiyo imefaulisha kwa asilimia 100, ambapo mwaka jana ilishika nafasi ya pili na mwaka huu imekamata nafasi ya kwanza mtawalia kiwiliaya.
“Ufaulu umepanda kutoka asilimia 66 mwaka 2010/2011 hadi asilimia 100 mwaka 2012/2013, ” aliongeza mkuu huyo.
Changamoto kubwa inayokabili shule ni pamoja na wazazi na walezi kusuasua kuchagia chakula shuleni kunakopelekea shuleni, kwani wanafunzi wanalazimika kwenda majumbani kula chakula na hatimaye kukosa masomo.
"Wito wangu kwa wazazi na walezi wachangie chakula cha wanafunzi ili waweze kula shuleni mchana hapa hapa, kuliko kwenda nyumbani ili kupunguza utoro na kuongeza mahudhurio kwa wanafunzi darasani," aliseam mwalimu mkuu huyo.

Wakati huohuo, imeelezwa kuwa ufaulu wa mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa mwaka 2013 umepanda kwa masomo yote kwa asilimia 19.89 ikilinganishwa na ilivyokuwa kwa mwaka uliopita. Kwamba, wakati mwaka jana wahitimu waliopata asilimia 100 walikuwa asilimia 30.72, mwaka huu wameongezeka kuwa asilimia 50.61.
Pia, somo ambalo watahiniwa hao wamefaulu zaidi katika mtihani wao ni  Kiswahili ambapo ufaulu ni  asilimia 69.06 huku wakiwa wamefeli zaidi kwenye somo la Hisabati ambalo ufaulu upo chini kwa asilimia 28.62.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dk. Charles Msonde alisema wanafunzi 427,606 walifanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013 huku kiwango cha udanganyifu kikizidi kudhibitiwa hivyo kupungua.
Alisema NECTA imefuta matokeo yote ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kwa watahiniwa 13, ambao walibainika kufanya udanganyifu kwenye mtihani au kurudia pasipo ruhusa ya Baraza. Watahiniwa waliofutiwa mwaka jana ni 293.
Alisema kati ya wanafunzi hao, 844,938 waliofanya mtihani huo wamepata alama zaidi ya 100 katika alama 250: ”Idadi hiyo ni sawa na asilimia 50.61. Kati yao wasichana walikuwa 208,227 (sawa na asilimia 46.68) na wavulana 219,379 sawa na asilimia 55.01,” alisema.
Dk. Msonde alisema katika ufanyaji wa mtihani huo, pia walikuwepo watu wenye ulemavu, ambapo wasichana walikuwa 219 na wavulana 257.
Alisema matokeo hayo yatapelekwa maeneo yote husika ili mchakato wa upangaji shule ukifanyika kwa watahiniwa wote waliofaulu mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi.
Kuhusu usahihishaji mitihani, Dk. Msonde alisema ili kujiridhisha na usahihi wa zoezi la usahihishaji wa kutumia mfumo wa kompyuta (Optical Mark Reader - OMR), sampuli za karatasi 20,795 za majibu ya watahiniwa wa shule 200 kutoka wilaya 48 zilichukuliwa kutoka shule za mikoa tisa ya (Iringa, Kagera, Shinyanga, Manyara, Njombe, Mbeya, Morogoro, Katavi na Tanga) na kusahihishwa kwa mkono: ”Ulinganifu baina ya alama za watahiniwa zilizopatikana kwa kusahihishwa kwa mkono na zile zilizotokana na usahihishaji wa mfumo wa kompyuta ulifanyika na kubaini kompyuta ilikuwa sahihi,”alisema.
Amesema makosa yaliyojitokeza katika karatasi zilizosahihishwa kwa mkono ni kuweka pata pale ambapo kuna kosa ama kuweka kosa pale ambapo kuna pata, makosa ambayo kwenye usahihishaji wa kutumia kompyuta hayakuwepo. Source: http://www.wavuti.com

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...