Skip to main content

WATANZANIA MILIONI 5 HATARINI KUTOPIGA KURA MWAKANI

Na Friday Simbaya, Songea
Katibu Mkuu wa Chadema Dkt. Wilibrodi Slaa amesema zaidi ya watu milioni tano (5m) nchini Tanzania hawataweza kushirika kupigakura ya maoni ya katiba ya rasimu ya pili kwa  kupigiakura kutokana na mbalimbal ikiwemo kukosa shahada za kupigiakura imefahamika.
Dkt. Slaa alisema kuwa watu wengi waliofikisha miaka kumi na nane (18) na waliopoteza shahada hizo ama kwa kuuza au kupoteza hawatashirika kupigakura ya maoni ya katiba.
Hayo yalisema leo wakati wa Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Tamasha vilivyopo Namihoro, wilayani Songea vijijini mkoani Ruvuma, wakitokea Mbamba Bay na Mbinga, ikiwa ni kuashilia mwanzo wa opresheni M4C PAMOJA Daima inayofanyika nchini nzima.
Alisema ili watu wengi waweze kushiriki kupigakura ya maoni ya katiba kikamilifu ni lazima daftari ya wapigakura nchini liboreshwe.
“Tunaiomba serikali kupitia Tume ya Uchaguzi Nchini (NEC) ianze zoezo la kuboresha daftari ya wapigakura ili watu wengi washiriki katika kupigakura ya maoni ya katiba na hatimaye Uchaguzi Mkuu wa 2015,” alisema Dkt. Slaa.
Aliwaomba wananchi wa Jimbo la Peramiho kushiriki kikamilifu katika chaguzi za serikali za mitaa zinazo tarajia kufanyika mwaka huu ili kuweza kuchaguwa upinzani kikiwemo chama cha Chadema.
Alisema kuwa kwa sasa maisha ya wanachi ni magumu pamoja kwamba nchi imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi lakini wananchi wake bado ni masikini kwa sababu ya viongozi kukosa moyo wa uzalendo.
Gharama za maisha inapanda kila siku hasa gharama za matibabu hospitali hususan hospitali binafasi ni kubwa na ukizingatia Peramiho haina hospitali ya serikali ambaye ni mkombozi wa wanyenge.
Alisema kuwa endapo chama chake cha Chadema kitafanyikwa kushika madaraka katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kitu cha kwanza ni kuuza ndege ya serikali amabye anatumia na rais na kununua helikopta nyingi zinazo fikika kila mahala kuliko ndege ya rais inayotua viwanja sita tu.
Aiongeza kuwa kutumia ndege ya serikali ni gharama kuliko kutumia helikopta kwa sababa ni rahisi kufanya mikutano kumi na nne kwa siku kwa sababu ya kutumia helikopta.

MALENGO YA OPERESHEN
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe alisema operesheni hiyo imezingatia mwaka 2014 kuwa na historia ya matukio ya kisiasa nchini, ambayo chama kinahitaji kujipanga kukabiliana nayo.
Aliyataja matukio hayo kuwa ni pamoja na Bunge Maalumu la Katiba linalotarajiwa kuanza rasmi mwanzoni mwa mwezi ujao.
Hivyo, alisema chama kimeona kuwa kuna ulazima wa kuliandaa Taifa kwa ajili ya kulikabili tukio hilo.
Alisema matukio mengine ni uchaguzi wa serikali za mitaa na kura ya maoni, ambayo itapigwa na wananchi kuamua ama kuikubali au kuikataa rasimu ya pili ya katiba mpya.
Kutokana na hilo, Mbowe alisema wanatumaini kuwa daftari la kudumu la wapigakura litatumika katika kuendesha kura ya maoni.
Hivyo, alisema wameona ni lazima waliamshe Taifa kuhusu kujiandikisha katika daftari hilo.
Alisema tangu mwaka 2010, daftari la kudumu la wapigakura halijaboreshwa.
Kutokana na hali hiyo, alisema itakuwa ni ndoto za serikali kufikiria kwamba Watanzania watarudi kuitumia katiba ya mwaka 1977 inayotumika hivi sasa baada ya kuwa tayari wamekwishaikataa.
Mbowe alisema matukio mengine ya kisiasa yanayotarajiwa kujiri mwaka huu, ni uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 27 nchini.

Alisema kati ya kata hizo, Chadema imesimamisha wagombea kwenye kata 26 baada ya mgombea wao katika Kata ya Mtae, mkoani Tanga kushindwa kurejesha fomu za kuomba kuwania kiti hicho katika mazingira ya kutatanisha.
Mbowe alisema katika mwaka huu pia kunatarajia kufanyika uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Kalenga kuziba nafasi iliyoachwa wazi kufuatia kifo cha Dk. Mgimwa.
Alisema pia katika mwaka huu watakuwa na uchaguzi wa ndani ya chama, hivyo wameona ulazima wa kuwaandaa wana-Chadema kushiriki uchaguzi huo.
Alisema pia Watanzania watakuwa na uchaguzi mkuu mwakani, hivyo wameamua kuutumia mwaka huu kukazia maandalizi kwa ajili ya ushiriki wao katika uchaguzi huo.
Mbowe alisema watatumia fursa hiyo kuibua kashfa na mambo yote yanayowakera wananchi katika maeneo yao.
Kwa mujibu wa Mbowe, operesheni hiyo ambayo itakuwa ya wiki mbili, itaendeshwa kwa njia ya mikutano ya hadhara na ya ndani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...