Skip to main content

NEC: Hakuna kura ya maoni bila daftari jipya

Rais Jakaya Kikwete akipokea Katiba Inayopendekezwa kutoka kwa Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma juzi. Katikati ni Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein. Picha na Edwin Mjwahuzi 

Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema haitaendesha uchaguzi wa aina yoyote, wala kuitisha kura ya maoni hadi kazi ya kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura itakapokamilika.
Kauli ya NEC imekuja siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta na kulitaja suala la uboreshaji wa daftari la hilo kama mambo matatu yanayoiweka kura ya maoni kupitisha Katiba hiyo njiapanda.
Mambo mengine ni Sheria inayotaka kura hiyo ipigwe ndani ya siku 84 baada ya Katiba inayopendekezwa kuchapishwa na kufanyiwa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva alisema jana kwamba kuendesha uchaguzi bila kuboresha daftari hilo ni kuongeza malalamiko kwa wananchi na wadau, hususan vyama vya siasa.
“Msimamo wetu (NEC) ni kuwa bila daftari kuboreshwa hatuko tayari kuendesha uchaguzi wowote na hata huo wa kura ya maoni,” alisema na kuongeza:
“Sasa tuna takriban vijana milioni 2.3 ambao wamefikisha umri wa kupiga kura ... lakini kuna watu waliokufa, vyote hivi vinatakiwa kuboreshwa kwanza na sisi Tume hatuko tayari, naomba muwaambie wananchi.”
Kuhusu hoja kwamba NEC itumie daftari lililopo kama ambavyo wamekuwa wakifanya katika uchaguzi mdogo mara kwa mara pale mbunge anapofariki dunia, Jaji Lubuva alisema tume yake haitaki yajirudie malalamiko ambayo imeyapata kupitia uchaguzi wa aina hiyo.
“Katika Uchaguzi wa Kalenga, Arumeru Mashariki na Chalinze, tulilalamikiwa sana kuhusu matumizi ya daftari hili, hivyo kutokana na malalamiko hayo yaliyotoka kwa vyama vya siasa, hatutaki tena kupata mengine kama hayo, ndiyo maana nasema muwaambie wananchi kwamba hatutaendesha chaguzi zozote hadi pale tutakapoboresha daftari,” alisema Jaji Lubuva.
Kuhusu lini kazi ya kuboresha daftari hilo itaanza, Jaji Lubuva alisema: “Tunasubiri vifaa vifike na vitakapofika tu tutaanza mara moja.”
Kauli ya Rais Kikwete
Akizungumza juzi katika sherehe ya makabidhiano ya Katiba inayopendekezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, Rais Kikwete alielezea maeneo matatu yenye utata ambayo yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi ili kufanikisha hatua hiyo.
Alisema suala la kwanza ni ratiba iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao ambayo inaonyesha mchakato wa kuandika upya Daftari la Wapiga Kura utakamilika Mei 2015. (MWANANCHI)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...