Skip to main content

WANAWAKE 512 WAGUNDULIKA NA KANSA YA SHINGO YA KIZAZI

MKOA wa Iringa umeweza kuchunguza kina mama 11,223 na kati hawa wanawake 512, (sawa na asilimia 4.6) waligundulika kuwa na mabadiliko ya awali na kupewa tiba katika kipindi cha kuanzia Januari 2014 mpaka Januari 2015.

Hayo yalisemwa hivi karibuni na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi, Mkoa wa Iringa, Adam Swai wakati wa mkutano wa kufunga na kutoa tathmini ya mradi wa kuhamasisha jamii kuhusu huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa shingo ya kizazi.

Alisema kuwa haya ni mafanikio makubwa yanayohitaji kuendelezwa na kuongeza kuwa wanawake 6,322, sawa na asilimia 56 walichunguzwa kwa jihudi za Shirika la Bristol Myers Squibb Foundation (BMSF) kupitia Taasisi ya T-MARC Tanzania.

Alisema kuwa utekelezaji wa mradi huu hapa Iringa, walengwa wakuu wa mradi walikuwa ni wanawake wenye umri wa miaka 30 hadi 50 katika maeneo ambayo wanajamii wako hatarini kupata saratani ya mlango wa kizazi kutokana kiwango cha maambukizi ya VVU kuwa juu.

“Walengwa wengine walikiwa makundi yote yenye ushawishi kwa walengwa wakuu katika uchunguzi wa afya zao, ili wawahamisishe kufanya maamuzi wa kupata huduma za uchunguzi na matibabu. Wanaume pia walishirikishwa katika mradi huu,” alisema Swai.

Alisema kuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazokumbwa na tatizo kubwa la saratani ya mlango wa kizazi duniani.

Asilimia 25 ya wanawake wa Tanzania wako hatarini kupata saratani ya mlango wa kizazi katika maisha yao, na saratani ya mlango wa kizazi ni mojawapo ya sababu zinazosababisha vifo vya wanawake nchini, alisema.

Takiwimu kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road inaonyesha katika wa wagonjwa wa saratani wanaopekwa katika taasisi hiyo kila mwaka, zaidi ya wagonjwa 5,000 wanatatizo la saratani ya mlango wa kizazi. 

Wataalamu wa mambo ya saratani wamegundua kuwa kuna uwiano mkubwa kati ya saratani ya mlango wa kizazi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

Takimwi za utafiti wa viashiria vya UKIMWI na Malaria nchini zinanaonesha kuwa Mkoa wa Iringa ni wa pili nchini kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya VVU.

Haya hivyo, katibu tawala msaidizi huyo alisema kuwa serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inafanya juhudi mbalimbali katika kupambana na saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake.

“Hii ni kwa sababu saratani ya mlango wa kizazi inatibika. Ila tu ili iweze kutibika, ni muhimu kuwa saratani hii igundulike katika hatua zake za awali, ” alisisitiza Swai.

Kwa upande wake, Meneja Ufualiaji, Tathmini na Utafiti kutoka T-MARC Tanzania, Dkt. Benjamin Kamala alisema kuwa mradi huu ulifadhiliwa na Shirika la Bristo Myers Squibb Foundation (BMSF) kupitia Pink Ribbon Red Ribbon (PRRR); ulitekelezwa nchini Tanzania kwa ushirikiano na mashirika matano ambayo ni T-MARC Tanzania, Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA), Asasi ya Tanzania Youth Alliance (TAYOA) na mtandao wa wadau wa UKIMWI Mbeya (MHNT).



Alisema kuwa mradi pia ulihusisha vituo mbalimbali vya afya ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Iringa, Hospitali ya Lugoda, Kituo cha afya Ipogolo, Hospitali ya Tosamaganga, Kituo cha afya Marie Stopes, Hospitali ya Mafinga, Kituo cha afya Usokami na Hospitali ya Ilula.



“Huu ni mwendolezo wa juhudi za wadau mbalimbali kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake wa Tanzania,” alisema Dkt Benjamin.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...