Skip to main content

CHIKU ABWAO NA MWANAHAMISI MUYINGA WASHINDA KURA MAONI ACT WAZALENDO...!

Mgombea Daudi Masasi aliyepata kura 21, agoma kusani matokeo kutokana na alichodai kuwa hajaridhishwa na  mchako.

Mgombea Chiku Abwao  aliyepata kura 25, akisani matokeo. 


ALIYEKUWA Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chiku Abwao ameshinda kura za maoni za chama cha ACT Wazalendo ikiwa ni siku chache toka ajiunge na chama hicho.

Ushindi mwembamba wa kura 25 alizopata dhidi ya mgombea mwenzake Daudi Masasi aliyepata kura 21, umemuweka katika nafasi ya kuteuliwa na chama chake hicho kipya kuwania ubunge wa jimbo la Iringa Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa baadaye mwaka huu.

Kabla ya kujiunga na ACT Wazalendo, Abwao alipania kugombea ubunge katika jimbo la Isimani kupitia Chadema, lakini kwa kile alichoita hila zilizokuwa zikifanywa dhidi yake na mbunge wa jimbo la Iringa Mjini anayemaliza muda wake, Mchungaji Peter Msigwa ndoto yake hiyo imekoma.


Kabla ya kushinda kura hizo za maoni Abwao alisema Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe anatarajia kuja mjini Iringa Jumapili Agosti 9 kwa lengo la kumtambulisha rasmi kwa wakazi wa mjini Iringa.

Alisema Kabwe atakayeambatana na aliyekuwa Mbunge wa Kasulu, Moses Machali na Afande Sele na viongozi wengine wa ACT atafanya mkutano mkubwa katika viwanja vya Mwembetogwa jumapili hiyo.

Wakati, aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Kalenga kupitia chadema Mwanahamisi Muyinga ameshinda kura za maoni za kugombea ubunge katika jimbo hilo kupitia chama cha ACT Wazalendo kwa kupata kura zaidi 20.

Mwanahamisi aliwashinda wagombea wenzako watatu na kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa kura za maoni uliyofanyika leo.

Hata hivyo, Mwanahamisi wamewashukuru wajumbe kwa kumpingia kura pamoja na wale ambao hawakumpigia kura na kuwaomba washirikiane katika kuleta maendeleo katika jimbo la Kalenga.

Wakati huohuo, Mwanahamisi amesema atachukua fomu pia ya kuwania ubunge viti maalum kupitia chama hicho kupitia jimbo la kalenga.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...