Skip to main content

KIPINDI CHA 'TUWALINDE WATOTO WETU' KURUKA TENA ALHAMISI HII, CLOUDS TV


Mmiliki na mwendeshaji wa kipindi cha Tuwalinde Watoto Wetu, Janet Mwenda.

Na Rabi Hume, Modewjiblog

Kipindi cha Tuwalinde Watoto Wetu kilichokuwa kikirushwa na Clouds TV, Alhamisi ya wiki hii kinatarajiwa kuanza tena kuonekana kupitia Clouds TV Alhamisi ya Disemba 10, saa tatu kamili usiku.

Akizungumza na Dewjiblog, Mmiliki na mwendeshaji wa kipindi hicho, Janet Mwenda amesema kuwa kipindi cha Alhamisi hii kinatarajiwa kuja na kitu kipya tofauti na vile walivyokizoea kuonekana hapo awali na hivyo kuwataka watazamaji kukaa tayari kuona kipindi bora kuhusu watoto na changamoto wanazokutana nazo.

Amesema lengo la kipindi hicho ni kuwakumbusha wazazi na walezi majukumu yao kwa watoto wao na hatari wanazoweza kukutana nazo pindi wasiposimamiwa vizuri na watu wanaoishi nao na kupitia kipindi hicho wanaweza kuona maisha wanayokutana nayo watoto hao pindi wanapokuwa nje ya familia zinazowalea.

“Kuna mambo jamii inakuwa haiyaamini kama yanatokea na tunachofanya ni kujaribu kuionesha jamii ni mambo gani yanawatokea watoto wanapokuwa mtaani na tunachotaka ni wazazi watambue hatari hiyo na waweze kuwalea vizuri watoto awe wa kwako au wa mwenzako,” amesema Janet.

Akizungumzia kipindi cha Alhamisi hii, Janet amesema kipindi cha wiki hii kitakuwa kinamuhusu kijana wa miaka 16 aliyekuja Dar es Salaam kutafuta maisha baada ya kutoroka nyumbani kwao na kujiunga na makundi mabaya ya vijana ambayo yalipelekea kuanza kujiingiza katika vitendo vya kimapenzi na wanawake wanaofanya biashara ya kuuza mwili na kuwa katika hali ya hatari ya kupata magonjwa ya zinaa.

Kujua kilichofuata baada ya kujiingiza katika vitendo hivyo na hali aliyonayo sasa kijana huyo usikose kutazama kipindi hicho alhamisi hii, Disemba 10 kupitia Clouds Tv!!!

USIKOSEEE!!


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...