Skip to main content

Wateja wa Tigo, AzamTV na LigaBBVA kwenda kuangalia mechi ya Barcelona bure



Mtendaji Mkuu wa Azam TV, Rhys Torrington (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Promosheni ya kujishindia safari ya kwenda kushuhudiamechi ya Ligi Kuu ya Hispania maarufu kama La Liga, kati ya Deportivo la Coruna na Barcelona Machi mwaka huu . Katikati yake ni Meneja Promosheni wa Tigo Pesa, Mary Rutta.Kulia kwake Mkuu wa Idara ya Masoko ya Azam TV, Mgope Kiwanga .Promosheni hiyo ya ushirikiano wa Tigo Pesa na Azam TV, inaanza rasmi leo hadi Machi 13 na washindi wawili watakwenda Hispania.




Tigo, Azam Media na LigaBBVA leo wametangaza ushirikiano baina yao ambao utawapa fursa watumiaji wa huduma Tigo Pesa
wanaonunua vifurushi vya michezo vya AzamTV kupata nafasi ya kusafiri bure bila malipo kwenda kutazama mechi ya ligi kuu kati ya miamba wawili wa Hispania – Barcelon na Deportivo la Coruna
– itakayofanyika Aprili mwaka huu.

Akiongea katika uzinduzi wa promosheni hiyo leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Promosheni wa Tigo Pesa, Mary Rutta amesema, “Kwa kufahamu mapenzi makubwa waliyonayo watanzania kwa mpira wa miguu hasa ligi kuu ya Hispania, Tigo imeungana na Azamtv na LigaBBVA ili kuwapa watanzania, hususan wateja wa Tigo Pesa fursa hii adimu na bure ya kusafiri na kwenda kutazama mechi kati ya Barcelona and Deportivo la Coruna itakayochezwa Aprili 17.”

Rutta alisema: “Mtumiaji wa Tigo Pesa anachohitaji kufanya kushinda fursa hii ni kuhakikisha kimoja kati ya vifurishi vikuu vya AzamTV kipo hewani (Pure, Plus, Play) na hapo atakuwa ameingia katika droo ya kumpata mshindi wa kwenda kushuhudia mechi hii ya kusisimua. Tunapenda kuwahimiza wateja wa Tigo watumiaji wa huduma ya Tigo Pesa kuchangamkia fursa hii ya kusafiri bila malipo kwenda Hispania.”

Tigo, kwa mujibu wa Meneja wa Promosheni wa Tigo Pesa huyo, ina zaidi ya wateja milioni tano waliojisali katika huduma ya Tigo Pesa waliopo kila kona nchini Tanzania

Akiongea katika uzinduzi huo. Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media, Rhys Torrington alisema, “Kama kawaida yetu, malengo yetu daima ni kuwapa kilicho bora zaidi wateja. Nchini Tanzania tunafahamu ni jinsi gani watu wanavyopumua, kula na kuishi mpira wa miguu na michezo kwa ujumla. 

Hii ni sababu iliyotupa msukumo wa kuleta LigaBBVA ambayo ni mojawapo katika ligi bora duniani kwa mashabiki wengi Tanzania ili kukata kiu yao ya mpira wa miguu.

Alisema “nafasi kama hizi hazijitokezi kila mara kushuhudia maajabu ya Messi, Neymar na Suarez yakitokea”. 

Tunapenda kuwahimiza mashabiki wote wa mpira wa miguu nchini Tanzania kutumia fursa ya kipekee kutimiza kutumiza ndoto zao katika maisha.” Mbali na washinfi wawili watakaosafiri kwenda nchini Hispania katika kipindi cha promosheni hii, aidha zitatolewa zawadi mbalimbali kwa washindi zikiwemo jezi asili za timu ya Barcelona, mipira ya miguu, mipira, tisheti, kalamu, miwani ya jua na zawadi nyinginezo. Ili kushinda zawadi. watazamaji wa mechi za LigaBBVA kupitia AzamTV watahitajika kupiga simu kabla ya mechi kuanza na wakati wa mapumziko na kujibu maswali yatakaokuwa yanaulizwa. 

Torrington alisisitiza “ LigaBBVA ambao tunashirikiana nao, wamefurahishwa na mapokezi mazuri ya watanzania kwa ligi ya ligi ya Uhispania kuanzia siku ya kwanza, na katika kuunga mkono promosheni hii wametukabidhi vifaa vyenye nembo ya LigaBBVA vitakavyotolewa kwa kwa washindi wa kila wiki na tunaamini huu ni mwanzo wa mambo makubwa yajayo.”





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...