Skip to main content

WAZIRI UMMY MWALIMU APOKEA MSAADA WA FEDHA WA MIL 220, KWA MATIBABU YA WAGONJWA WA MOYO


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Ally Mwalimu leo Machi 2.2016, amepokea msaada wa fedha kwa ajili ya kuwezesha matibabu ya wagonjwa wa moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo kwa msaada huo, jumla ya watoto 101, wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo katika taasisi hiyo kwa gharama za fedha hizo zilizotolewa na Jumuiya ya Kihindu waishio Dar es Salaam ijulikanayo kama BAPS Charity, kwa kuguswa kwao na kutoa msaada mkubwa na upendo waliouonyesha kwa watanzania wanaosumbuliwa na maradhi ya moyo.

Wiziri Ummy amebainisha kuwa, kiasi cha msaada unaotolewa utawezesha wagonjwa wapato hao kupatiwa matibabu ya moyo hivyo kuwa, faraja kubwa kwa wagonjwa waliokuwa wakisubiria huduma hizo kwa muda mrefu kutokana na kushindwa gharama za matibabu yake.

Aidha, kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Mohamed Janabi amepongeza kwa msaada huo kwani utasaidia kutoa matibabu kwa watoto hao 101, huku pia taaisi yake ikikabiliwa na changamoto ya wagonjwa wengi ambapo amezitaka taasisi na wadau wengine kujitokeza kuchangia ilikupunguza wagonjwa wanaosubiria kupatiwa matibabu hasa upasuaji.

Prof. Janabi ameeleza kuwa, matibabu ya wagonjwa wa moyo yana gharama kubwa kwani kwa mtoto mmoja ndani ya nchi yanafikia hadi Milioni nne (Mil 4) huku kwa nje ya nchi matibabu hayo yakifikia hadi Milioni 16, gharama hizo ni kubwa hivyo wadau na taasisi binafsi zimeombwa kujitokeza ilikuokoa maisha ya wagonjwa wengi hasa watoto ambao wapo katika taasisi hiyo na mikoa mingine.
Tazama MO TV, kuona tukio hilo hapa:
Kusoma hotuba ya Waziri hapa:
waziri ummy5


Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Mohamed Janabi akisoma taarifa fupi juu ya magonjwa wagonjwa wa moyo wanaopatiwa matibabu katika taasisi hiyo na namna walivyojipanga kutoa matibabu ya upasuaji kwa watoto hao 101, waliolipiwa gharama za matibabu kutoka BAPS Charity. Wengine ni Waziri wa Afya, Mh. Ummy Mwalimu pamoja na viongozi wa BAPS Charity.


Waziri Ummy Mwalimu akiongea na mmoja wa wazazi waliokuwa katika tukio hilo la kukabidhiwa fedha kiasi cha Mil 220, kwa ajili ya wagonjwa wa moyo 101, ambao wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya JKCI.


Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akipata kumjulia hali mtoto Zahara Seleman Muna (10) ambaye anasumbuliwa na magonjwa ya moyo. Hata hivyo Waziri Ummy Mwalimu amejitolea kama Waziri kuhakikisha atawasaidia watoto hao katika kutimiza ndoto zao ikiwemo kuwasomesha na masuala mengine kupitia Wizara yake ambayo yenye dhamana, Waziri Ummy aliguswa na watoto hao kutokana na ndoto zao walizokuwa nazo ikiwemo kusoma zaidi.


Mwenyekiti wa taasisi ya BAPS Charity, Subhash Patel, akizungumza machache kuhusiana na mchango huo wa Milioni 220, kwa ajili ya matibabu ya watoto 101, ambapo pia aliomba wadau wengine kujitokeza kuchangia ilikuisaidia Serikali katika kuhakikisha uhai kwa wagonjwa wa moyo hasa watoto hapa nchini.


Bw. Alfred D. Dafi mkazi wa Karatu akiwa amembeba mtoto wake, Beatrice Alfred (13) akitoa shukrani zake kwa Waziri wa Afya, Mh. Ummy Mwalimu kwa kuweza kuchukua majukumu ya kumsaidia mtoto wake katika masuala ya kumsomesha na mambo mengine kama Waziri mwenye dhamana. Waziri amechukua jukumu ya kuwasaidia watoto hao, kutokana na kuguswa na ndoto walizonazo ikiwemo kusoma wafike mbali. Mtoto huyo Beatrice hadi sasa anasoma darasa la sita, katika shule ya Sumawe, iliyopo Karatu.


Dk. Naiz Majani, ambaye ni daktari wa watoto wa magonjwa ya moyo akitoa ufafanuzi kwa wanahabari juu ya matatizo ya magonjwa ya moyoo ambapo amebainisha kuwa kati ya asilimia 10, pekee magonjwa ya moyo yanabainika kwa mwanamke huku miongoni mwa wazazi wanaozaa watoto wenye matatizo ya moyo ni wale waliokosa chanjo mbalimbali ikiwemo ya Lubela na mambo mengine.


Watoto Beatrice Alfred (13) na Zahara Seleman Muna (10) wakiwa katika picha ya pamoja. Waziri wa Afya, Mh. Ummy Mwalimu ameamua kujitolea kuwasaidia kutimiza ndoto zao ikiwemo suala la kuwasomesha na mahitaji mengine kama Waziri mwenye dhamana. Kushoto ni Baba wa mtoto Beatrice, Bw. Alfred Dafi ambaye anatokea Karatu.


Waziri Ummy Mwalimu akimpa pole dada wa Zahara Seleman Muna (10), Editha Foi,(kulia) aliyekuwa akilia kwa uchungu baada ya Waziri Ummy Mwalimu kuamua kujitolea kuwasaidia watoto hao iliwatimize ndoto yao ya elimu na mahitaji mengine kama Waziri Mwenye dhamana.


"Uchungu wa Mama", Waziri Ummy Mwalimu akiwa na watoto Beatrice na Zahara ambao wanasumbuliwa na magonjwa ya moyo, ambapo baada ya kuwajulia hali na kuguswa na ndoto zao za kielimu, Waziri Ummy Mwalimu ameguswa na watoto hao na kuamua kuwasaidia katika elimu na mambo mengine kama Waziri mwenye dhamana.

.

Waziri Ummy Mwalimu akiwa akipeana mkono na baada ya kukabidhiwa hundi ya sh. Mil 220, iliyotolewa na taasisi ya BAPS Charity kwa ajili ya kusaidia matibabu ya watoto 101, wa magonjwa ya moyo waliopo katika taasisi ya JKCI. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog/MO TV).


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...