Skip to main content

MCHUNGAJI MPELI AMPONGEZA MAGUFULI KWA KUMJUA MUNGU


Mbeya: Mkurugenzi na kiongozi wa taasisi ya dini ya Daily Bread Life Ministry Tanzania, Mchungaji James Mpeli Mwaisumbe amewasihi watanzania kumuombea Rais Dkt John Pombe Magufuli ili aweze kuliongoza taifa kwa haki, amani na upendo.

Alisema kuwa ili Tanzania iweze kusonga mbele, waislamu, wakristo,viongozi wa siasa, serikali na watanzania kwa ujumla lazima waliombee taifa na viongozi wake kwa Mungu ili kuweza kudumisha amani na mshikamano viliyopo.

Mchungaji Mpeli alisema hayo wakati wa sherehe ya kumuaga Mchungaji Raphael Mwasifiga wa Kanisa la Baptist, Kanani lililopo Sinde Makunguru, Mwanjelwa jijini Mbeya. 

Mchungaji huyo mwalikwa alisema kuwa anavutiwa na kiongozi wa nchi kwa sababu ni mcha Mungu na katika maneo yake kumi anayozungumza hakosi kumtaja Mungu.

Alisema kuwa taifa ni kitu cha muhimu kuliko vya vyama siasa na kuwaomba wakristo, waislamu viongozi wa siasa na serikali kuliombea taifa ili amani na mshikamano ambayo havipatikani Afrika isipokuwa Tanzania viweze kudumu.

“Kiongozi mwenye hofu ya Mungu ni yule ambaye anajinyenyekeza na kujishusha kama Yesu Kristo alivyo jinyenyekeza msalabani,” alisema Mchungaji Mpeli.

Alisema kuwa Tanzania imekuwa ikisifiwa na mataifa mbalimbali kuwa ni nchi yenye amani duniani lakini amani, upendo na mshikamano viweze kudumu ni lazima viongozi wawe na hofu na kuwa wanyenyekevu kwa kuutafuta uso wa Mungu. 

Aidha, Mchungaji Mpeli katika ibada maalumu ya kumuaga mchungaji mwenzake Raphael Mwasifiga, iliyofanyika tarehe 29.08.2016 alisoma neno la Mungu kutoka katika Kitabu cha 2 Mambo ya Nyakati 7: 14. 

Neno la Mungu linasema hivi, “ ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” 

Kuhusu hali ya siasa nchini, Mchungaji Mpeli Mwaisumbe amevitaka vyama vya siasa vitangulize maslahi ya taifa mbele na vyama vya siasa baadaye ili kuepusha vurugu kutokea nchini.

Alisema kuwa vyama vya siasa vinatakiwa kukaa chini kutafuta suluhu ya mvutano unaoendelea kuhusu operesheni ya Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) ili kuepusha vurugu kutokea nchini. 

Mchungaji huyo alimuomba pia msajili wa vyama vya siasa nchini kuwa asichoke kukemea na kuvionya vyama vyote vya siasa bila upendeleo wowote. 

Kwa upande wake, Mchungaji Mstaafu Raphael Mwasifiga wa Kanisa la Baptist Kanani la Makunguru Sinde, Mwanjelwa mkoani Mbeya alisema kuwa serikali na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wanatakiwa kukaa chini kutafuta suluhu ya mvutano unaoendelea kuhusu operesheni ya Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) ili kuepusha vurugu kutokea nchini maandamano hayo yatakapofanyika. 

Mchungaji huyo, alisema ili kuepuka machafuko yanayoweza kutokea wakati wa kutekeleza operesheni hiyo Septemba mosi, mwaka huu, huku Jeshi la Polisi likisema litauvunja Ukuta ni vyema pande zote mbili zikajadiliana na kupata muafaka. 

"Hakuna jambo lililoshindikana mezani, tunaiomba serikali ikae mezani na viongozi wa Chadema ili kumaliza tofauti," alisema. 

Mchungaji Mwasifiga alizaliwa mwaka 1953 katika kijiji cha Lukule Kiwira Tukuyu wilayani Rungwe, mkoani Mbeya akiwa ni mtoto wa saba na wa mwisho katika familia ya Mzee Mwasifiga.

Mchungaji Mwasifiga alikuwa mchungaji mwanzilishi wa Kanisa la Baptist Kanani Makunguru Sinde maeneo ya Mwanjelwa jijini mbeya tangu mwaka 1992 na alimshukuru Mungu kwa kumaliza salama.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...