Skip to main content

WANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI WAANZA MITAHANI YAO LEO



NA KAROLI VINSENT
Jumla ya wanafunzi 435,221wa kidato cha pili nchi nzima leo wametarajia kuanza mitihani yao ya taifa ya kidato cha pili.
Ambapo kati yao wavulana ni 214,013 sawa na asilimia 49.17 na wasichana 221,208 sawa na asilimia 50.83.
Mbali na hao wapo wanafunzi wenye mahitaji maalum ambao watahiniwa wasioona ni 67 na watahiniwa wenye uoni hafifu ni 306 ambao watapewa maandishi ya karatasi hukuzwa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Katibu mkuu wa Baraza la Mitihani nchini,Dkt Charles Msonde amesema mtihani huo ambao umeanza mapema hii leo ambao unatarajia kumalizika Nombemba 25 ya mwaka huu.

Amesema mtihani huo unalengo la kuwapima uwezo na uelewa kwa wanafunzi katika yote wajifunzayo kwa miaka miwili ya masomo yao huku wanafunzi wanaofeli wanakosa nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu.

Dkt Msonde amesema maandalizi yote ya mtihani huo yamekamilika ikiwemo kusambazwa kwa mitihani itakayotumika katika upimaji huo pamoja na nyaraka muhimu katika mikoa na halmashauri zote ndani ya Tanzania bara.
Hata hivyo,Dkt msonde amesema Jumla ya wanafunzi 10,045,99 wanatarajia kuanza mitihani ya darasa la nne mwaka huu siku ya tarehe 23 na 24 Novemba ambapo kati yao wavulana ni 507,732 sawa na asilimia 48.54 na wasichana na 538,267 sawa na asilimia 51.46.
Pamoja na hayo dkt msonde amewataka wanafunzi pamoja na wasimizi kutohusika na vitendo vya udanganyifu huku akisema hatua kali za kisheria kwa waliohusika
Pamoja na hayo Dk Msonde amefafanua kuwa mafunzo ya ualimu wa shule ya msingi ngazi ya stashahada yamefutwa lakini wanafunzi waliopo vyuoni watamalizia masomo yao kwa muda uliobaki.

Dk Msonde amesema mafunzo hayo ya walimu yataendelea kwa utaratibu wa zamani ambao ulikuwa ngazi ya cheti.

Amesema usimamizi wa mitihani hiyo itakuwa chini ya Necta kama ilivyokuwa zamani badala ya Nacte.

"Wanafunzi walio vyuoni wataendelea na mafunzo hayo, isipokuwa kuanzia mwaka huu hatutadahili kwa ngazi ya diploma, tutadahili ngazi ya cheti kama ilivyokuwa zamani," amesema Dk Msonde.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...