Skip to main content

HATIMAYE MPEMBA WA MAGUFULI ABURUZWA MAHAKAMANI,NI YULE JANGILI WA MENO YA TEMBO



Hatimaye Vinara wanaodaiwa kujihusisha na mtandao wa kukusanya, kuuza vipande 50 vya meno ya tembo, vyenye thamani ya Sh. milioni 392.8 wamepandishwa katika mahakamani wakikabiliwa na mashtaka manne ya kuhujumu uchumi akiwamo, Yusuf Ali maarufu kama Shehe ama "Mpemba" (35).

Mbali na "Mpemba", washtakiwa wengine n mfanyabiashara mkazi wa Mrimba, Mkoani Morogoro, Charles Mrutu maarufu Mangi Mapikipiki ama Mangi Mpare (37), wakazi wa Dar es Salaam, Benedict Kungwa (40) Jumanne Chima maarufu Jizzo ama JK (30), Pius Kulagwa (46) na Dereva wa Vikindu, Pwani Ahmed Nyagongo (33).

Washtakiwa wote walisomewa mashtaka yao leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.Wakili wa Serikali Paul Kadushi, alidai kuwa kati ya Januari, mwaka 2014 na Oktoba, mwaka huu maeneo tofauti Mkoani Dar es Salaam, Morogoro, Iringa, Tanga na Mtwara washtakiwa wakiwa na wenzao ambao bado hawajashtakiwa mahakamani, walijihusisha na matukio ya uhalifu.

Ilidaiwa pia, washtakiwa walijihusisha kukusanya, kuuza vipande 50 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Dola za Kimarekani, 180,000 (sawa na Sh. 392,817,600) mali ya Serikali ya Tanzania, bila kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Upande huo wa Jamhuri ulidai katika shtaka la pili, Oktoba 26, mwaka huu eneo la Mbagala Zakhem Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam, washtakiwa walikutwa na vipande 10 vya meno ya tembo vikiwa na uzito wa kilo 13.85 vyenye thamani ya Dola za Kimarekani, 30,000 (sawa na Sh. 65,469,600) mali ya Serikali ya Tanzania, bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Shtaka la tatu na la nne, ilidaiwa kuwa kati ya Oktoba 27 na 29, mwaka huu na eneo la Tabata Kisukulu, Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam, washtakiwa walikutwa na vipande 40 vya meno ya tembo vikiwa na uzito wa kilo 69.56 vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 150,000 (sawa na Sh. 327,348,000) mali ya Serikali ya Tanzania, bila kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Kadushi alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba Jamhuri inaandaa nyaraka mbalimbali ikiwamo maelezo ya mashahidi pamoja na vilelezo kwa ajili ya kuwasilisha taarifa katika Mahakama Maalum ya kesi za Kuhujumu Uchumi na Rushwa (mafisadi).

Hakimu Simba alisema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama yake haina mamlaka ya kusikiliza kesi za kuhujumu uchumi.

Kesi hiyo itatajwa Desemba Mosi, mwaka huu na washtakiwa wamepelekwa mahabusu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...