Skip to main content

WASHINDI WA SINGELI IRINGA WAOMBA KUUNGWA MKONO


Innocent aka Lusso Mnyama 



Isihaka aka Msangazi baharia





WASHINDI wa mashindano ya kuimba singeli mkoa wa Iringa, Isihaka Msangazi ‘Baharia’ na Innocent Chanafi’ Lusso Mnyama’ wamewataka wadau kuwaunga mkono katika harakati zao kuupandisha muziki huo nyanda za Juu Kusini.

Wakizungumza na SIMBAYABLOG jana mara baada ya kushinda mashindano ya kuimba sengeli katika mkoa wa Iringa yaliandaliwana kituo cha Radio cha Nuru Fm, Mshindi wa kwanza, Isihaka na Innocent walisema kuwa muziki huo unakuwa kwa kasi zaidi kutokana na ubora wake na kuonyesha uhalisia wa kitanzania zaidi.

Walisema kuwa wawekezaji wakiwa wengi katika aina hiyo ya muziki ni lazima ajira iongezeke kupitia fani ya muziki hasa huu wa singeli ambao kwa sasa unazidi kuteka hisia za mashabiki wengi hasa katika sherehe mbalimbali.

Kwa upande wake mshindi wa kwanza, Isihaka Msangazi alisema kuwa ushindi wake umekuja kutokana na kujituma kwa bidii katika mazoezi na kuupenda muziki huo ambapo lengo ni kufika mbali zaidi katika kuwakilisha mkoa wa Iringa na taifa kwa ujumla.

Alisema kuwa mshindani wake alikuwa mkali lakini baada ya majaji kuona anastahili ushindi alimpongeza mshindani wake Lusso Mnyama kwa kuweza kukubali hali halisi ya mashindano hivyo natoa wito kwa wadau kutuunga mkono katika harakati za kuinua muziki wa singeli nyanda za juu kusini.

. “Watu waje wengi kuusaidia muziki huu kuanzia mapromota na wengineo kwa kuwa wananchi wanaupenda na kazi ni kuuinua zaidi na sio kuuona ni kama muziki wa kawaida kwani kwa sasa wengi wanachukulia kama mziki wa kihuni kitu ambacho sio kweli” alisema

Alisema kuwa hadi sasa anatarajia kuingia studio na kuandaa vibao mbalimbali vyenye staili ya singeli ambavyo vitakuwa moto wa kuotea mbali ndani ya nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla.

Naye Innocent Chanafi ambaye alikuwa mshindi wa pili katika mashindano hayo alisema kuwa asilimia kubwa ya watu kwa sasa wako katika muziki wa bongo fleva lakini baada ya mashindano hayo ana uhakika Iringa itakuwa moja ya mikoa yenye waimbaji wengi wa muziki wa singeli.

Alisema kuwa mashindano hayo ya kuimba singeli mkoa wa Iringa yamemsaidia sana kuweza kutambua ni kwa kiasi gani kwa sasa yanaweza kuwa moja ya aina ya muziki ambao utaubeba uhalisia wa Mtanzania Kimataifa kutokana na vionjo vyake.

Alisema kuwa aina hii ya uimbaji inaonekana kuwa ni aina mpya ambayo inaweza kuutambulisha muziki wa kitanzania nje ya nchi hasa kutokana na aina yake ya uimbwaji, uchezaji hata mashabiki wake kwani wengi wao ni vijana ambao ni taifa la kesho katika kusogeza mbele maendeleo ya Tanzania.

Alisema hadi sasa anatarajia kutoa nyimbo mbili za ‘Shem Lake’ na 'Baki na Mimi ambazo amefanya katika studio za Familly rekodi chini ya produza Yuda Tz zilizoko jiji Dar es salam.










Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...