Skip to main content

JPM ASEMA TANZANIA HAINA NJAA, NI PROPAGANDA ZA WANASIASA NA...



HOTUBA YA RAIS MAGUFULI LEO SIMIYU. 
Rais Dk. John Magufuli leo hii akiwa mkoani Simiyu amesema kwamba Tanzania hakuna njaa na kwamba anayejua kama nchi ina njaa ni yeye mwenyewe.

"Anayejua kuna njaa nchi hii ni Rais, mimi ndiyo ninayejua wapi kuna njaa na wapi hakuna.Tanzania hii haina njaa wala watu hawana njaa," anasema Rais JPM kutoka Simiyu

"Wanaotangaza kuna njaa ni watu wanaolipwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kusema nchi ina njaa na ukame wa kuua watu na mifugo.

"Yapo magazeti yanayotumiwa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kusema Tanzania kuna njaa. Kuna mfanyabiashara mmoja ana tani elfu 25 za mahindi bandarini anataka aingize bila kodi kwa kisingizio cha njaa Tanzania," amesema.

Rais anasema ameagiza alipe kodi na asipitishe mahindi hayo bure kwa kisingizio cha njaa, kwa sababu Tanzania haina njaa.

"Kuna mfugaji mwingine walimlipa hela wanasiasa huko Mvomelo,akaenda mbele ya TV na kusema ana mifugo inakufa kwa ukame. Nimeagiza wamwambie auze hizo ng'ombe ili aepukane na ukame. Huwezi kuwa na ng'ombe karibu elfu na zaidi na wanakufa ng'ombe 16 unaanza kulialia badala ya kuuza upate hela ya kula na ujikimu kimaisha," amesema Rais Magufuli.

Rais anasema hatapeleka chakula Simiyu na Bariadi eti kisa ukame na akaongeza kwamba wananchi walitakiwa kujua kama mvua ni ndogo basi walime mazao yanayostahimili ukame na si kulazimisha kulima mahindi yanayohitaji mvua nyingi.

JPM anasema msema ukweli ni mpenzi wa Mungu na yeye anasema ukweli kuwa hataleta chakula popote kwa sababu ni wanasiasa na wafanyabiashara ndio wananunua magazeti kutangaza njaa.

Rais kamuumbua Dk. Titus Kamani, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu anayemtaka Rais aruhusu kuingiza mifugo kwenye hifadhi, wakati yeye akiwa Waziri wa Mifugo wakati wa JK hakufanya hivyo, na akahoji sasa kama siyo unafiki ni nini?

JPM anasema yeye sio mnafiki, hataruhusu mifugo kuingia kwenye hifadhi kwa sababu ya sifa za kisiasa huku akiharibu mazingira.

Rais anasema Watanzania walizowea kuambiwa maneno "matamu matamu" na wanasiasa huku muda ukienda bila kuwa na maendeleo.Yeye anataka Watanzania wasahau maneno matamu matamu. Ataongea ukweli tu, tena ukweli mchungu hata kama utawaudhi watu, kama ni jiwe atasema jiwe na sio mchanga mgumu uliokusanyika pamoja.

Rais amewaomba Watanzania wazidi kumuombea, kwani wapo "wapinzani" wake wanamsimanga kwa kununua ndege, na wakati kwa miaka mingi Tanzania haikuwa na ndege,na hao wanaomkosoa ndio hao hao wanaokimbilia kuzipanda.

Baadaye Rais akamuita Mhandisi wa Maji wa Mkoa wa Simiyu ili aje aelezee mpango wa Maji kutoka Ziwa Victoria kuja mkoa wa Simiyu na Wilaya zake.

Mhandisi hakutoa majibu mazuri. Akaja RAS ambaye akasema kikwazo ni mlima wa Ngasamo ambao una madini ya Nikel ambao ndio ilipaswa kuwa na tank la kuleta maji.

Eneo hilo tayari kuna muwekezaji na hawawezi kuweka tank.
Rais ameamuru mgodi huo usipewe leseni na huyo muwekezaji apewe taarifa kuwa huo mgodi haupo tena na watu wapewe eneo la kuweka Tank.

Amemuagiza Kamishna wa Madini aifute leseni na ujumbe umfikie Waziri wa Madini na autekeleze.

Na mwisho Rais amesisitiza watu wafanye kazi, hakuna wa kugawiwa chakula bure. Hawezi akawasomeshea watoto bure, ajenge barabara, anunue ndege, ajenga hospitali na kuweka madawa kstika hospitali, alete huduma ya maji na bado watu wakae tu na kusubiri eti serikali itawatafutia chakula.

"Watu wafanye kazi ili wapate chakula na si kusubiri chakula cha serikali. SERIKALI YANGU HAITATOA CHAKULA, NINAPOSEMA SILETI CHAKULA SILETI KWELI, WALA SIMUNG'UNYI MANENO NA SITALETA KWELI, MLIZOEA MANENO MATAMU SASA MIMI SINA MANENO MATAMU," alisisitiza Rais Magufuli.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...