Skip to main content

VIONGOZI WA VIJIJI WAHOFIA UTEKELEZAJI WA KODI YA MAJENGO



Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji, watendaji wa kata, tarafa pamoja na wakuu wa idara wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa vijiji wakati wa kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)







Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahuninga, Kata ya Mahuninga wilayani Iringa, mkoani Iringa Lonjino Mkwele akimuuliza swali Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela (hayupo pichani) kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa vijiji wakati wa kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)





VIONGOZI wa vijiji vyote wa Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa waagizwa kusoma mapato na matumizi ili kuwarahisishia wananchi kufahamu jinsi fedha zao zinavyotumika na kutoa fursa kwa wananchi kupata nafasi ya kuhoji ili kujiridhisha pale wanapokuwa na mashaka.

Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa (DC), Richard Kasesela wakati wa mkutano na wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji, watendaji wa kata, tarafa pamoja na wakuu wa idara wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa .

Kikao hicho cha kazi kililenga kuwakumbusha wenyeviti na watendaji wa vijiji na Kata kutambua majukumu yao na kuyapatia majibu sawia pamoja na swala zima la ukusanyaji mapato .

DC Kasesela ameagiza kufanyanyika uchunguzi ili kubaini kama kuna watendaji waliohamishwa kazi na wanatuhumiwa kuhujumu mapato ya serikali na michango ya wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo kurudishwa haraka. 

Mkuu huyo wa Wilaya amewaagiza watumishi wote wa serikali ngazi ya Vitongoji, Vijiji na Kata kufanya kazi kwa haki, Usawa na uwazi na kiwashirikisha wananchi katika kila jambo linalohusu vipaombele vya maeneo yao. 

Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa vijiji waliohudhuria katika mkutano huo wamempongeza mkuu wa Wilaya ya Iringa kwa kufanya mkutano uliyolenga kuwakumbusha majukumu yao pamoja na kuwakutanisha kwa pamoja.

Wakati huohuo, watendaji wa vijiji, watendaji wa kati pamoja na watu wa mapato wamekumbushwa kukusanya kodi ikiwemo kodi ya majengo.

Hata hivyo baadhi ya viongozi wa vijiji wamekuwa na wasiwasi kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa kusema wananchi wengi katika maeneo hawana uelewa juu ya kodi hiyo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahuninga, Kata ya Mahuninga wilayani Iringa, Lonjino Mkwele alitaka kujua Kodi ya Majengo itatozwaje.

Kwa upande wake, Mdhamini wa Wilaya ya Iringa, John Brayson aliwaomba wananchi wote kulipa kodi ya majengo kwa maendeleo ya uchumi.

Alisema wameanza zoezi kwa kuthamini na ukusanyaji wa kodi ya majengo na mchakataji wa taarifa za majengo umeanza katika jumla ya vijiji 133 vya wilaya pamoja na kata 28.

Brayson alisema kuwa wanapata changamoto katika kutekeleza sheria ya kodi ya majengo hasa maeneo ya vijiji hapo awali walikuwa hawatozwi.

ADHABU KWA ATAKAYESHINDWA KULIPA KODI YA MAJENGO

· Kutozwa faini ya asilimia 50 ya kodi yake.

· Asipolipa halmashauri imepewa mamlaka ya kukamata mali yenye thamni sawa na kodi na kuuza kufidia kodi hiyo.


Kodi ya majengo katika Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ilianza kutozwa mwaka 1983, katika kipindi hicho kodi hii ilitozwa katika maeneo ya majiji, manispaa, miji midogo na makao makuu ya halmashauri ya wilaya tu.

Lakini mwaka 2015 yalifanyika marekebisho ya sheria kuruhusu hata maeneo mengine ya halmashauri ya wilaya kutoza kodi ya majengo kwa kuthamini majengo kwa njia ya mkupuo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...