Skip to main content

ANSGAR CUP 2017 PERAMIHO, NGOMA 'INOGILE'





Na Alex Mapunda, Ruvuma

MWAKILISHI wa Kata ya Peramiho katika Mashindano ya Ansgar Cup ngazi ya Tarafa, timu ya Afya Fc imefanikiwa kuitandika bila huruma Kilagano Fc timu toka Kata ya Kilagano kwa kichapo cha bao 3-0.


Katika mchezo huo ambao Mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Simon Bulenganija, bao la kwanza la Afya Fc liliwekwa kimiani na mshambuliaji machachari Emanuel Kajana dakika ya 39 ambalo liliwachanganya wachezaji wa Kilagano FC na wakaanza kucheza kwa Tahadhari kubwa.

Dakika 15 za kipindi cha pili Kilagano Fc walicheza vizuri mno na walifanikiwa kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika lango la Afya Fc, lakini mambo yalikuwa tofauti baada ya mchezaji wa Afya Fc Shabiru Kinunga kuipatia timu yake hiyo bao la pili lililopeleka majonzi kwa Kilagano Fc mnamo dakika ya 60 ya mchezo.

Lakini Kabla ya mpira kumalizika mfungaji wa bao la kwanza Emanuel Kajana alishindilia msumari wa moto katika vidonda vya Kilagano Fc kwa kuipati Afya Fc bao la tatu kwa njia ya kichwa kunako dakika 88, bao ambalo lilikamilisha ushindi mnono wa bao 3-0 baada ya mwamuzi wa mpambao huo kupuliza filimbi ya mwisho kuashiria kwamba pambano limemalizika.

Katika mchezo wa mapema uliopigwa mishale ya saa nane mchana timu toka Kata ya Parangu ilikumbana na kipigo cha jumla ya bao 2-1 toka kwa Litisha Fc toka kata ya Litisha.

Kata zilizojitosa katika mashindano hayo ni Kata ya Peramiho, Litisha, Parangu, Kilagano, Lilambo, Maposeni, Mpandangindo pamoja na Liganga ambapo mechi za ufunguzi ilikuwa ni kati ya Litisha dhidi ya Parangu mishale ya saa nane mchana kisha saa kumi jioni Kilagano Fc wakakumbana na Peramiho (Afya Fc) kwenye uwanja wa Ansgar uliopo Peramiho B.

Mwaka huu zawadi zimeboreshwa toka shilingi 300,000/= kwa washindi wa kwanza hadi shilingi 400,000/= , 250,000/= washindi wa pili hadi shilingi 300,000 pamoja na 150,000/= washindi wa tatu hadi 200,000/= huku mchezaji bora akiambulia kifuta jasho cha shilingi 50,000/= hali ambayo imesababisha ongezeko la ushindani na kila timu shiriki inatamani kunyakua ubingwa wa mshindano hayo.

Ansgar cup ni moja ya ligi kongwe mkoani Ruvuma na imedumu kwa zaidi ya miaka 20, lengo kubwa la mashindano ya Ansgar yanayoandaliwa na mkurugenzi wa Hospitali ya Peramiho Dkt. Ansigar Stuffe OSB ni kuibua vipaji kwa wachezaji, burudani baada ya kazi, kuongeza soka la biashara kwa wafanyabiashara wa tarafa ya Peramiho n.k.

Baadhi ya wachezaji waliotokea Ansgar Cup ni pamoja ni Pato Ngonyani (MajiMaji na Yanga), Anold Nguruchi na wengineo wengi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...