Skip to main content

AVUNJWA MGUU KWA RISASI


Mkazi wa kitongoji cha Endevesi ,kata ya Oljoro wilaya ya Arumeru,Hwanga Ndaskoy(30)amefunjika mkuu wake wa kulia baada ya watu wanaodaiwa kuwa ni askari polisi mkoani Arusha, wapatao nane kumvamia na kumpigwa risasi ,akiwa shambani kwake .


Akizungumza kwa masikitiko nyumbani kwake, baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Mount Meru alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki moja,Ndaskoy ameeleza kwamba tukio hilo limetokea mnamo,Agost 31,mwaka huu majira ya saa saba wakati akivuna mahindi shambani kwake akiwa na familia yake.


Alisema kua alifuatwa na askari hao waliokuwa wamevalia kiraia na mmoja mwenye silaha akiwa amevaa sare za kipolisi.


Pia askari hao walikuwa wameongozana na mkazi mmoja wa kitongoji hicho aliyemtaja kwa jina la ,Yohane Palay aliyemtambua kuwa ni baba mkwe wake .



‘’Nilimsikia baba mkwe akiwaelekeza askari hao wanikamate huku akiwatahadhalisha kuwa mimi ni mkorofi na wasinisogelee nitawakata na sime jambo ambalo sio kweli,ndipo askari mmoja mwenye silaha aliponifyatulia risasi ya mguu na kuanguka chini’’alisema Ndaskoy 


Aidha alisema askari baada kumpiga risasi walimpakia kwenye gari lao na kumpeleka katika hospital ya Mkoa Mt,Meru ambapo walimweleza daktari kuwa ameanguka na pikipili Jambo ambalo si kweli.


Alieleza kuwa kabla ya tukio hilo ,Agost 26 mwaka huu ,aligombana na mke wa kaka yake aitwaye ,Jehova Baraka ambaye wanaishi jirani baada ya mbuzi kula mahindi yake yaliyokuwa nyumbani .


Alisema ugomvi huo ulienda mbali zaidi kiasi cha kutoleana maneno makali ,ambapo Jehova aliamua kwenda kwa baba yake mzazi aitwaye Yohane Palay na kutoa taarifa kuwa amepigwa na shemeji yake .


Palay aliamua kwenda kituo cha polisi cha Mbauda jijini hapa na kutoa taarifa juu ya tukio hilo,hata hivyo viongozi wa kitongoji hicho wakiwemo wazee wa ukoo waliingilia kati na kumtaka Palay alirejeshe nyumbani ili wazee wa ukoo walipatie ufumbuzi wa kudumu jambo ambalo waliafikiana.


Alisema Kikao cha ukoo kiliketi,agost 30 na kukubaliana kumaliza jambo hilo kwa kuwatoza faini za kimila wahusika wote wawili baada ya kubaini wote wanamakosa,hata hivyo walishangaa kesho yake agost 31 kufuatwa na polisi na kupigwa risasi.


Kwa upande wake,Palay alikiri kupeleka malalamiko yake kituo cha polisi ,Mbauda ,akidai kuwa mtoto wake,ambaye ni mke wa kaka yake na majeruhi alipigwa na kudhalilishwa. Hata hivyo aalikana kuwarubuni Polisi ili wampige risasi mtuhumiwa





Akizungumzia tukio hilo,kamanda wa polisi mkoa wa Arusha,Charles Mkumbo alisema kuwa anafuatilia undani wa tukio hilo ikiwemo kubaini ni askari gani walienda kwenye tukio hilo na kuahidi kulitolea ufafanuzi.


"Kwa kweli sina taarifa ya tukio kama hilo ila nitachunguza kama lipo nitalitolea ufafanuzi" Kauli ya Mkumbo.


Mkumbo alisema analifanyia uchunguzi jambo hilo kupitia wasaidizi wake na kuahidi kuchukua hatua kali iwapo itabainika hapakuwa na ulazima wa matumizi makubwa ya silaha ya moto kwa askari wake.


Na Woinde Shizza 





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...