Skip to main content

BOT YAPIGA MSASA VIZIWI MKOANI IRINGA KUHUSU NOTI HALALI




IRINGA: Viziwi mkoani Iringa wameishukuru Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa kuendesha mafunzo ya elimu ya umma ya utambuzi wa alama za usalama za noti halali. 

Walemavu hao walitoa kauli hiyo jana kwenye risala iliyosemwa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza, ambapo jumla ya viziwi 50 walipatiwa mafunzo ya utambuzi wa alama za usalama za noti halali. 

Walisema kuwa semina hiyo ni muhimu sana kwao kwa sababu itawawezesha kutambua noti halali na halisi kwa walemavu wa kusikia mkoani Iringa. 

Mafunzo hayo yaliandaliwa na kituo cha sanaa na utamaduni kwa viziwi Tanzania (KISUVITA) kwa kushirikiana na Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) mkoa wa Iringa. 

Akisoma risala mwenyekiti wa KUSUVITA, Habibu Mrope kwa niaba ya walemavu alishukuru BOT kwa kuwezesha mafunzo ikiwa ni mwendelezo wa zile, ambazo zimekwishafanyika katika mikoa ya Lindi, Dodoma, Singida, Ruvuma, Njombe, Shinyanga, Simiyu, Mwanza, Mara, Kigoma, Tabora na Kagera tangu mwaka 2010. 

KISUVITA ni asasi isiyo ya kiserikali na isiyolenga faida, iliyoanzishwa kwa ajili ya kuendeleza vipaji vya viziwi pamoja na upatikanaji wa haki za katika Nyanja mbalimbali za maisha kupitia sanaa ya utamaduni. 

Mrope alisema kwa wakati asasi, mashirika binafsi, vyama vya siasa, serikali na taasisi zake zikiendesha semina, makongamano, mikutano ya hadhara kwa ajili ya masuala mbalimbali katika tasnia ya afya, eleimu, utamaduni, uchumi na kijaamii, viziwi hawafikiwi na program hizo. 

Alisema kuwa mbaya zaidi hawashirikishwi katika masuala mbalimbali ikiwamo ya utoaji wa maamuzi katika ngazi mbalimbali za kiserikali, kifamilia na kadhalika na kwa sababu hiyo wanaendelea kubakia nyuma kulinganisha na makundi mengine ikiwamo ya ulemavu mwingine. 

Kwa upande wake, Meneja msaidizi, Idara ya uhusiano wa umma kutoka BoT makao makuu Vickoria Msina, alisema waliona ni muhimu kulielimisha kundi hilo, ili kuwawezesha kuepuka kubambikiziwa noti bandia kisha kuchukuliwa hatua za kisheria. 

Msina aliwataka viziwi na jamii nzima kuzingatia njia tatu za utambuzi wa noti halisi na bandia. 

Njia hizo ni pamoja na kuangalia, kushika na kutumia vifaa vinavyonunuliwa katika maduka ya umeme. 

Alisema kuwa, katika kuangalia noti halisi picha ya baba wa taifa, Mwalimu Julius Nyerere huonekana vizuri na nywele nyeupe, lakini katika noti bandia haonekani vizuri na picha huwa na weusi, na kuwa pia noti halisi mstari wake hung’aa na kucheza cheza huku katika noti bandia hauchezi hukaa tu. 

Alisema kuwa, katika alama ya kuangalia noti halisi ikiwekwa sambamba inaonyesha maua, lakini ikiinuliwa hayo maua huonyesha alama ya thamani ya noti husika. 

“Mfano kama ni noti ya shilingi 10,000 maua hayo ukiinua yataonyesha tarakimu ya shilingi elfu kumi, lakini bandia hata ukiinua itaonyesha maua tu” anasema. 

Aidha alisema kuwa, katika alama ya kuangalia, nyuma ya noti katika kichwa cha twiga, hela halali ukiichezeshachezesha kichwa hicho kinabadilika na kuwa kijani kisha dhahabu, lakini hela bandia inabaki dhahabu tu haibadiliki. 

Kuhusu njia ya pili ambayo ni ya kushika, anasema noti hushikwa sehemu mbili tu, ambazo ni kwenye pembe, ambapo hela halisi ikishikwa kwenye pembe itakwaruza lakini bandia itateleza tu. 

“Pia sehemu iliyoandikwa fedha halali kwa malipo ya shilingi fulani nayo hukwaruza ukipitisha dole gumba tofauti na bandia ambayo huteleza tu,” anasema. 

Mtaalam huyo anataja njia ya tatu ya utambuzi wa noti halisi na bandia kuwa ni ya kutumia vifaa vinavyouzwa katika maduka ya vifaa vya umeme ambavyo ni taa ya rangi (bulb) na taa maalum ya kuangalia noti bandia. 

Msina alisema kuwa, mbali na kuwafundisha viziwi namna ya kuzitambua na kuzitofautisha noti hizo, pia walemavu wasioona nao kuna alama zao ambazo wanazitambua pindi wanapogusa noti yoyote halali. 

Pamoja na elimu hiyo pia aliwataka wananchi kuzitunza vizuri fedha hizo ili zisichakae, maana zikichakaa husababisha serikali kushindwa kutekeleza kwa wakati miradi mbalimbali ya jamii, maana hulazimika kuchukua noti zilizochakaa kwenda kutengeneza hela nyingine, badala ya kuzipeleka kwenye matumizi ya miradi. Na Friday Simbaya, Iringa

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...