Skip to main content

USAID NAFAKA YATOA RUZUKU ZANA ZA KILIMO KWA WAKULIMA MKOANI IRINGA










Na Friday Simbaya, Iringa

MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amepongeza Mradi wa NAFAKA kwa juhudi za kuinua uchumi wa vikundi vya wakulima na kuleta maendeleo katika sekta ya kilimo. 

Alisema kuwa Kilimo kinatoa mchango mkubwa wa ajira kwa vijana na wanawake walioko vijijini na mijini kwa maendeleo yetu na Taifa kwa ujumla.

Masenza alisema hayo jana wakati wa kukabidhi zana za kilimo kwa wakulima katika vikundi vya uzalishaji, na kuongeza kuwa zana hizo za kilimo zitasaidia wakulima kuongeza tija, uzalisahji na kufanya shughuli za kilimo kwa wakati. 

Pia, alisema kuwa nyenzo hizo za kilimo zitawezesha vijana na wanawake kushiriki katika kilimo kwa mafanikio makubwa ikiwa pamoja na kukuza uchumi wa kipato katika ngazi ya kaya pamoja na kupunguza umasikini kwenye mkoa wa Iringa.

“Serikali inahimiza sana wakulima wadogowadogo, wakulima wakati na wakubwa kutumia zana bora za kilimo katika shughuli za uzalishaji mazao ili kuongeza tija na maeneo ya mashamba yanayolimwa na zana bora za kilimo,” alisema Masenza. 

Masenza alisema kuwa Mpango wa Ruzuku wa Zana za Kilimo unaotolewa na Mradi wa NAFAKA wa USAID, ni fursa muhimu kwa Vikundi vya wakulima.

Pia serikali itaendelea kuwaunganisha wakulima na vikundi vya wakulima kwenye fursa mbalimbali ambazo zinapatikana serikalini ikiwa ni juhudi za kuunga mkono Serikali ya Awamu ya tano (5) katika kuimarisha kilimo na kuongeza thamani ya mazao kwa kukoboa na kusanga badala ya kuuza kama nafaka au mali ghafi.

Kwa upande wake, Meneja Ruzuku wa Mradi wa NAFAKA wa USAID, Pius Tizeba alisema kuwa mradi umetoa ruzuku ya zana za kilimo yenye jumla ya thamani ya Tsh. 303,497,000/- kati ya hizo vikundi vya wakulima vimechangia jumla ya Tsh. 52,252,000/-.

Aidha vikundi tisa (9) kutoka wilaya za Kilolo na iringa vimepata ruzuku ya zana za kilimo yenye thamani ya Tsh. 74,930,000/-, ambapo vikundi vimechangia jumla ya Tsh. 9,938,000/-.

Tizeba alisema zana za kilimo ambazo vikundi vya wakulima toka wilaya za Kilolo na Iringa walikabidhiwa ‘Power Tiller’ nne (4) zenye thamani ya Tsh. 36,400,000/-,mashine za kukoboa na kusaga mahindi tatu (3) zenye thamani ya Tsh. 24,450,000/- na vifaa vya kinga wakati wa kupuliza viuatilifu mashambani vyenye thamani ya Tsh. 14,080,000/-.

Alisema kuwa pamoja na mafanikio ya vikundi vya wakulima kuweza kuchangia ruzuku kwa kupata za za kilimo, wanakabiliwa na changamoto za kukosa fedha za kujengea jengo la kuweka mashine za kusaga na kukoboa pamoja na kuunganisha umeme,kutokuwa na ujuzi wa kulima kwa kutumia ‘power tiller’.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...