Skip to main content

LIPULI FC YATAMBA KUICHAPA SIMBA SC

Wachezaji wa wakigombania mpira wa kona katika lango la timu ya Lipuli wakati wa mechi dhidi ya Singida United (jezi la rangi ya kijani) ya mkoani Singida katika Uwanja wa CCM Samora mjini Iringa Jumapili. Timu ya Lipuli ilishinda 1-0. (Picha na Friday Simbaya)

Mshambuliaji wa Timu ya Singida United Deus Kaseke mwenye jezi namba saba (7) mgongoni akijaribu kumtoroka Beki wa timu ya Lipuli FC Daruwesh Saliboko katika mechi iliyopigwa Jumapili katika Uwanja wa CCM Samora mjini Iringa. Lipuli FC iliishinda Singida United 1-0. (Picha na Friday Simbaya)


Mshambuliaji machachari wa Timu ya Lipuli ya mjini Iringa Malimi Busungu akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza ndani ya dakika 17 kipindi cha kwanza ya mechi dhidi ya Singida United jana (Jumapili) katika uwanja wa CCM Samora mjini Iringa. Matokeo mechi hiyo Lipuli FC dhidi ya Singida United yalikuwa 1-0. (Picha na Friday Simbaya)



Mashabiki wa Timu ya Lipuli FC wakisangilia timu ya kwa mavuvuzela dhidi ya Singida United ambapo timu yao iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika Uwanja wa CCM Samora mjini Iringa Jumapili. (Picha na Friday Simbaya) 





IRINGA: Timu ya Lipuli FC ya mjini Iringa imeomba mashabiki na wapenzi kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao itakaposhuka dimbani kuzichapa na Simba SC ya jijini Dar es Salaama Ijumaa wiki hii. 

Timu hiyo imetamba kuwa imejipanga kuibuka na ushindi katika mchezo wake wa Ijumaa dhidi ya Simba SC ya jijini Dar es Salaam unaotarajia kuchezwa katika uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini hapa. 

Kocha msaidizi wa Timu hiyo Selemani Matola alisema katika mchezo wa Ijumaa wiki hii timu hiyo inatarajia kuifunga Simba, ambapo watakutana na mchezaji wao wazamani Asante Kwasi aliyetimkia Simba. 

"Sisi benchi la ufundi tumelifanyia kazi jambo hilo na sasa tunajipanga kuhakikisha tunaibuka na ushindi katika uwanja wetu wa nyumbani, "alisema Matola. 

Kwa upande wake, Ofisa Habari wa timu hiyo Clement Sanga alisema ushindi katika mechi hiyo ni muhimu kama sehemu ya kujiweka katika nafasi nzuri timu yake lakini pia kupunguza machungu yaliyotokana na kipigo cha Jumatano wiki iliyopita dhidi ya Mwadaui FC ya Shinyanga cha mabao 2-1. 

Timu ya Lipuli ya mkoani Iringa inatarajia kumenyana na kisiki cha mpingo Simba SC ya jijini Dar es Salaam tarehe 20 Aprili mwaka. 

Simba ambao wanaoongza Ligi Kuu msimu wa 2017/18 kwa kuwa na alama 55 wakifuatia na wapinzani wao Yanga waoshika nafasi ya pili kwa kuwa na alama 47, hawajawahi kufungwa hata mechi moja tangu kuanza kwa ligi. 

Hata hivyo, Timu ya Lipuli ya mkoani Iringa imejihakikishia kubaki Ligi Kuu ya Vodacom Tanzabia Bara baada yakuibamiza Timu ya Singida United Jumapili wiki iliyopita katika mzunguko wa 25 kwa kupata alama 31 na kuendelea kushikilia nafasi ya saba (7) huku Singida United wakiwa na alama 37 nafasi ya tano (5). 

Jumapili iliyopita Lipuli FC walicheza na Singida United katika Uwanja wa kumbukumbu wa Samora mjini Iringa nakushinda 1-0, kupitia kwa mshambuliaji machachari Malimi Busungu dakika 17 ya kipindi cha kwanza cha mchezo. 

Uwanja wa Samora ulilipuka kwa shangwe kutoka kwa mashabiki baada ya mshambuliaji Busungu waliyevalia jezi namba 16 mgongoni kuitikisa nyavu ya Singida United. 

Timu ya Singida United inaoongezwa na Kocha Mkuu Mdachi Hans van der Pluijm aliyezaliwa tarehe 3 Januari mwaka 1949) ambaye pia ni golikipa mstaafu aliyewahi kuchezea timu ya Den Bosch FC katika ya mwaka 1967 na 1986, na baada ya kustaafu soka alikuwa meneja wa Timu ya Den Bosch mpaka 1995. 

Timu ya Lipuli ya mkoani Iringa imerejea ligi kuu Tanzania bara baada ya kupita miaka 17 tangu iliposhuka daraja na mkoa huo kukosa timu ya Ligi Kuu Vodacom kwa kipindi chote hicho. 

Kocha msaidizi wa zamani wa Simba raia wa Uganda Richard Amatre ndiye aliyeipandisha timu hiyo baada ya kusota nayo kwa miaka mitatu ikiishia katika nafasi za pili na tatu. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...