Skip to main content

WALIMU MANISPAA YA IRINGA WAMCHARUKIA MKURUGENZI KUHUSU MADENI YAO


WALIMU wa Manispaa ya Iringa wameomba Mkurugenzi wa Halmashauriya Manispaa ya Iringa kuwalipa madeni walimu wote fedha zao za uhamisho wanazodai, ambaz.o wanadai kwa muda mrefu. 

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) manispaa hiyo, Fotunatafatuma Njalale, alisema pamoja na serikali kusema kuwa haitaki kuzalisha madeni mapya ya walimu, bado kumekuwa na uhamisho wa walimu kwenda kwenye vituo vipya bila kulipwa fedha za uhamisho. 

Njalale alisema kuwa wapo walimu waliohamishiwa nje ya Walaya ya Iringa na walikwenda kuripoti kwa nauli zao na baadaye kurudi kudai posho za usumbufu nauli na usafiri wa mizigo yao, 

Alisema kuwa walimu hao wa Manispaa wanadai pesa ya usumbufu kutoka eneo moja kwenda nyingine, wakati wale walimu wa vijijini wanatakiwa kulipwa pesa ya usumbufu na kujikimu. 

Alisema madai hayo ni ya muda mrefu lakini hawajalipwa hata senti huku wakilazimishwa kwenda kwenye vituo vipya vya kazi kwa vitisho na kuonekana ni watoro. 

Njalale alisema kuwa kumekuwepo na taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari kwamba walimu wa manispaa ya iringa wameanza kulipwa madeni yao uhamisho kitu ambacho kimeleta taharuki kwa walimu. 

Alisema kuwa baada yakupata taarifa hiyo baadhi ya walimu wamekuwa wampigia simu kutaka ufafanuzi kuhusu walimu walianza kulipwa madeni yao. 

Alisema kuwa anao walimu baadhi yao walidaiwa kulipwa madeni yao uhamisho lakini wamekiri kwamba hawajaona kitu chochote kwenye akaunti zao. 

Aidha, Nipashe iliongea na baadhi ya walimu ambao hawakutaka majina yao yatajwe gazetini walisema kuwa mkurugenziwa halmashauri amekuwa kuwapa ahadi zisizotekelezeka. 

Walisema kuwa tangu wabadilishiwe vituo vyao vya kazi hawajalipwa hata centi tano licha mkuruguzi kuwaahidi kuwalipa pesa zao za usumbufu pamoja na zakujikimu. 

Kwa upande wake, kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Omari Mkangama alsiema kuwa ,Halmashauri ya Manispaa ya Iringa inendelea kuwalipa madeni watumishi hao waliohamishwa vituo vyao vya kazi. 

Akizungumza na wanahabari jana Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa huyo alisema kuwa wapo baadhi ya walimu waliohamishwa katika shule za msingi na sekondari ambao walihamishwa na tayari wameanza kulipwa stahiki zao. 

Mkangama alisema kuwa katika walimu ambao walihamishwa toka Sekondari kwenda shule za msingi kati ya hao Halmashauri imewalipa asilimia 65 ya madai yao ambayo ni zaidi ya milioni 69 zimelipwa. 

Alisema kuwa halmashauri yake inaendelea kuwalipa watumishi wote wastaafu pamoja na walimu wa shule za msingi na sekondari waliohamishwa na tunaendelea kufanya mchakato wa malipo na wote watalipwa. 

Hata hivyo, alisema kuwa walimu hao walihamishwa kutokana na mrundikano wa walimu (over staffing) katika kituo kimoja, kwa mfano kituo kimoja kina walimu sita wote wanafundisha somo moja. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...