Skip to main content

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa




Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari.

Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa.

Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti.

“Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithibati. Hatua hii ni muhimu katika kulinda taaluma, uadilifu na hadhi ya uandishi wa habari nchini,” amesema Kipangula.

Amefafanua kuwa ithibati si adhabu bali ni chombo cha kitaaluma kinacholenga kuhakikisha anayefanya kazi ya uandishi wa habari ana sifa, maadili na uelewa wa misingi ya taaluma hiyo, sambamba na kuwalinda waandishi halali dhidi ya manyanyaso au changamoto wanapotekeleza majukumu yao.

Aidha, amewahimiza waandishi wa habari kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya uandishi wa habari, akisisitiza kuwa bodi iko tayari kushirikiana nao kwa karibu katika kujenga tasnia imara, yenye weledi na inayoheshimika ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Iringa Press Club (IPC) Frank Leonard amesema ujio wa Bodi ya Ithibati Iringa ni fursa muhimu kwa waandishi wa habari wa mkoa huo kupata elimu ya moja kwa moja, kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu ithibati na haki zao za kitaaluma.

“Tunaiomba JAB kuendelea kusogeza huduma hizi hadi ngazi za chini zaidi ili waandishi waliopo wilayani na vijijini nao wanufaike,” amesema.



Waandishi wa habari waliohudhuria kikao hicho wamepongeza hatua ya bodi kufika mikoani, wakisema itasaidia kupunguza mkanganyiko kuhusu ithibati, kuongeza uwajibikaji na kuimarisha mshikamano ndani ya tasnia ya habari.

JAB imeeleza kuwa itaendelea kufanya ziara katika mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na waandishi wa habari, kuhamasisha ithibati halali na hatimaye kuinua viwango vya taaluma ya uandishi wa habari Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...