Skip to main content

Mradi wa Maji Warejesha Tabasamu kwa Wanafunzi wa Jamhuri

 



Mbarali. Wanafunzi wa Shule ya Msingi Jamhuri iliyopo Kijiji cha Ilongo, Kata ya Ilongo wilayani Mbarali mkoani Mbeya, wameanza kunufaika na mradi wa maji safi uliotekelezwa na Rufiji Basin Water Board kupitia Mradi wa NBS-USANGU.

Kabla ya utekelezaji wa mradi huo, wanafunzi walilazimika kutembea zaidi ya kilometa tatu kutafuta maji, hali iliyokuwa ikiathiri mahudhurio yao, kuongeza uchovu na kuchelewesha masomo. Wengine walilazimika kufika shuleni wakiwa wamechoka, jambo lililopunguza umakini darasani.

Kupitia mradi huo, kisima kirefu kimechimbwa na maji kusambazwa moja kwa moja shuleni pamoja na kwa wananchi wa maeneo jirani, hatua iliyoboresh­a mazingira ya kujifunzia na kuimarisha usalama wa wanafunzi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi hivi karibuni , Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Jenifer Sanga, alisema upatikanaji wa maji ndani ya shule ni mabadiliko makubwa kwa ustawi wa wanafunzi.

“Hii ni faraja kubwa kwetu. Sasa wanafunzi hawatapoteza muda kutafuta maji na wataweza kujikita zaidi katika masomo yao. Tunaamini hata ufaulu utaongezeka kwa sababu mazingira yameboreshwa,” alisema Sanga.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Ilongo, Benjamini Mwakalonge, alisema mradi huo umekuwa suluhisho la changamoto ya muda mrefu ya maji katika eneo hilo.

“Tunashukuru kwa kuifikia jamii yetu. Maji haya yatasaidia si wanafunzi tu bali pia wananchi wanaozunguka shule hii. Sasa tunapata maji karibu na makazi,” alisema Mwakalonge.

Hata hivyo, ushirikiano kati ya Serikali ya Japan na Tanzania umeendelea kuimarika kupitia miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi, hususan katika maeneo ya vijijini yenye changamoto za miundombinu ya maji.

imelezwa kuwa uwekezaji katika sekta ya maji ni hatua muhimu katika kuboresha afya, elimu na ustawi wa jamii kwa ujumla, akisisitiza kuwa upatikanaji wa maji safi na salama ni msingi wa maendeleo endelevu.

Mradi huo umetkelezwa na Rufiji Basin Water Board kupitia Mradi wa Kuimarisha Mbinu za Asili za Kijamii za Usimamizi wa Vyanzo vya Maji na Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi (NBS-USANGU), unaofadhiliwa na Serikali ya Japan kupitia World Bank.

Kupitia mradi huo, wanafunzi wa Shule ya Msingi Jamhuri sasa wananufaika si tu kwa kupata maji karibu, bali pia kwa kuimarika kwa mazingira ya usafi shuleni, jambo linalotarajiwa kupunguza magonjwa yanayotokana na ukosefu wa maji safi.

Baadhi ya wanafunzi waliozungumza kwa furaha walisema awali walikuwa wakichelewa kufika shuleni au kushindwa kuhudhuria vipindi vya asubuhi kwa sababu ya jukumu la kutafuta maji, lakini sasa wana muda wa kutosha wa kujifunza na kushiriki kikamilifu katika shughuli za shule.

Uongozi wa shule umeeleza kuwa uwepo wa maji utasaidia pia kuanzisha bustani za shule na miradi midogo ya lishe, itakayochangia kuboresha afya za wanafunzi na kuongeza ari ya kujifunza.

Kwa ujumla, mradi huo umeonekana kuwa kichocheo cha mabadiliko chanya katika Kijiji cha Ilongo, ukionesha namna usimamizi endelevu wa rasilimali za maji unavyoweza kuleta matokeo ya moja kwa moja katika sekta ya elimu na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...