Skip to main content

ASKARI POLISI AJIUA KWA KUJIPGA RISASI


Na Friday Simbaya,

Iringa



ASKARI polisi amefariki dunia baada ya kujipiga risasi mbili chini ya kidevu, kifo kinachosadikiwa kuwa kinahusiana na wivu wa kimapenzi baina yake na askari mwingine.

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla alisema askari huyo alijipiga na kufa papo hapo Julai 8, mwaka huu saa 3:00 usiku katika eneo la makazi ya mkuu wa mkoa wa Iringa eneo la Gangilonga, manispaa ya Iringa.

Alimataja askari huyo kuwa ni G13 Mashauri (24) ambaye kabla ya kujiua alikuwa kwenye lindo eneo la benki ya CRDB ambako aliingia lindoni saa 12:00 jioni Julai 8, mwaka huu na kutoka saa 1:30 usiku kuelekea nyumbani kwa askari wa kike.

Akielezea tukio hilo Mangalla alisema inadaiwa kuwa zamani Mashauri na Zahara walikuwa na uhusiano wa kimapenzi ambao hata hivyo waliachana kutokana na kutokuwepo na maelewano mazuri baina yao.

Alisema baada ya kuachana kila mmoja aliendelea na mambo yake na hadi siku ya tukio hilo ambapo Mashauri alikuwa akifuatilia nyendo za askari huyo aliyekuwa na mahusiana ya kimapenzi awali.

Mangalla alisema askari huyo aliondoka kwenye lindo lake na kuelekea eneo la Mafifi, Kihesa nyumbani kwa askari wa kike (WP 7137) aitwae Zahara ambako alikwenda baada ya kufika alibisha hodi na kufunguliwa mlango.

“Baada ya kufunguliwa alimkuta Zahara amekaa na kijana mmoja aitwae Sunday Tumaini mfanyakazi wa Bayport akawatishia, ndipo askari wa kike alipiga kelele kuomba msaada, askari mwingine aliyekuwa amepanga kwenye nyumba hiyo alitoka na kusaidia”alisema kamanda huyo.

Alisema askari aliyekuja kumsaidia Zahara, alimnyang’anya silaha aliyekuwa nayo Mashauri na baada ya kunyang’anywa aliondoka eneo hilo na kwenda kwenye lindo jingine eneo la Gangilonga kwenye Rest House ya Polisi ambako aliwakuta askari wengine ambao alianza kuzungumza nao.

Alisema baada ya kuzungumza nao ghafla alimnyang’anya silaha askari mwenzake na kuondoka nayo kwenda kwenye eneo alilojiulia kwa kujipiga risasi mbili chini ya kidevu.

Hata hivyo Mangalla alisema kuwa taarifa za awali za kujiua kwa askari huyo zinaonyesha alijiua kutokana na wivu wa kimapenzi lakini polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi wa tukio hilo.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...