Skip to main content

KITIMUTIMU JIMBO LA IRINGA MJINI

BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mjini Iringa katika Jimbo la Iringa Mjini, kesho wameahidi kuanza kurudisha kadi za chama hicho katika ofisi za matwi yao ikiwa ni matokeo ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kumuengua katika kinyang’anyiro cha ubunge, Fredrick Mwakalebela aliyeshinda kura za maoni za chama hicho katika jimbo la Iringa Mjini.






Katika kura hizo, Mwakalebela alimshinda kwa kura 3, 897 na mpinzani wake wa karibu Bi.Monica Mbega aliyepata kura 2,989.






NEC imemuengua Mwakalebela katika mbio hizo za kuusaka ubunge katika jimbo hilo kumeelezwa kuhusishwa na kashfa ya rushwa inayomkabili.






Baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa baadhi ya wanachama walioapa kurudisha kadi za chama hicho na kumuunga mkono mgombea wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), mwandishi wa habari hii jana alitembelea baadhi ya matawi ya chama hicho mjini hapa na kushuhudia makundi ya wanaCCM wakijipanga na kuendelea kuwashawishi wenzao kesho kuzirudisha kadi za CCM katika ofisi za matawi yao.






Matawi hayo ni pamoja na Kichanngani, Kihesa, Wilolesi, Soko Kuu la Mjini Iringa, Mshindo na Igumbilo.






Baadhi ya wanaCCM hao walisema maamuzi ya NEC yamemtoa kafara Mwakalebela ambaye taarifa zilizopo zinaonesha kwamba hakuwahi kukamatwa akitoa rushwa katika kinyang;anyiro hicho cha kura za maoni.






“Taarifa za Takukuru zinadai kwamba kwa kupitia mke wake ambaye naye hakukamatwa akifanya hivyo, Mwakalebela alitoa rushwa ya Sh 100,000 kwa wanachama 22 wa kijiji cha Mgongo, waliokuwa wamekusanyika nyumbani kwa Gwido Sanga wakimsikiliza wakati akitangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo,” alisema David Butinini wa tawi la Mtwivila.






Naye Julie Sawani wa tawi la Kichangani, alisema wakati Mwakalebela akienguliwa kwa madai hayo ya rushwa, inashangaza kuona NEC hiyo hiyo imeyapitisha majina ya Basil Mramba na Andrew Chenge ambao wanatuhuma kubwa za rushwa.






Alli Mduba wa tawi la Kihesa alisema uamuzi wa CCM wa kuwataka wanachama wote washiriki katika kura hizo umekiwezesha chama hicho kujua wagombea wanaokubalika katika mbio hizo za uongozi, hata hivyo akasema maamuzi yaliyofanywa na NEC dhidi ya Mwakalebela majibu yake watayapata Oktoba 31, siku ya Uchaguzi Mkuu.






Mohamed Kassim wa wilolesi alisema, kesho jumatatu wanachama watarudisha kadi zao za CCM katika ofisi ya tawi katika tukio ambalo pia watalitumia kumtangaza rasmi mgombea watakayemuunga mkono.






Naye Edgar Sanga wa Igumbilo alisema wanaCCM watamaliza jazba zao za mgombea wao kuenguliwa kwa kumpigia kampeni na kura mgombea wa Chadema. Mchungaji Peter Msigwa.






“Mwakalebela ndiye aliyekuwa chaguo letu vijana, na wananchi wote wa jimbo la Iringa Mjini bila kujali rangi, itikadi, dini na makabila yao, tumesikitishwa na uamuzi wa NEC,” alisema mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Anna Michael wa tawi la Miyomboni.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...