Skip to main content

MWAKALEBELA KORTINI LEO



ALIYEKUWA Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Frederick Mwakalebela na mkewe Selina Mwakalebela wamefikishwa mahakamani na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) Mkoa wa Iringa huku wakisindikizwa na umati mkubwa wa makada wa Chama cha cha Mapinduzi (CCM) na wananchi wa Manispaa ya Iringa.


Umati ulifurika mahakamani hadi kupelekea wasikilizaji wengine kusikilizia kesi inayowakabili huku wakiwa nje ya mahakama ya hakimu mkazi wa mkoa wa Iringa.


Umati huo unakuja siku chache baada ya Halmashauri kuu ya CCM (NEC) kumuengua Mwakalebela aliyeshinda kwa kupata kura 3,897 dhidi ya Mbunge aliyepita Monica Mbega aliyepata kura 2989 ambaye ameteuliwa na NEC.




Akisoma mashtaka hayo mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Iringa, Gladys Barthy, waendesha mashtaka wa Takukuru,Prisca Mpeka na Imani Mizizi walisema mshitakiwa namba moja na mbili kwa pamoja walitoa hongo ya sh. 100,000 kwa Gwido Sanga ili awagawie wajumbe ambao waliitwa kwenye kikao.


Mpeka alisema Julai 20 katika kijiji cha Mgongo Mwakalebela anadaiwa kuitisha kikao nyumbani kwa Sanga ambacho kilihudhuriwa na wajumbe wa CCM 22 ambapo baada ya hotuba Selina Mwakalebela alitoa Sh100,000 kwa Sanga ili awagawie wajumbe waliohudhuria.


Mpeka alisema washtakiwa hao kwa pamoja, walitoa rushwa kinyume cha sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) kinachokwenda sambamba na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka mwaka 2010 kifungu namba 21 (1) (a) na kifungu cha 24(8).


Washitakiwa wote walikana shitaka na kuachiwa kwa dhamana baada ya wadhamini kutimiza masharti yaliyowekwa na Mahakama.
Baada ya mabishano ya muda mrefu kati ya upande wa Mshaki ukiongozwa na Mizizi na wakili wa Mshakiwa, Basil Mkwata mahakama iliridhia sifa za wadhamini baada ya wadhamini wawili taarifa zao kutofautiana.


Alisema baada ya wadhamini kukamilisha masharti mahakama ilitoa dhamana ambayo masharti yake yalikuwa walitakiwa kuwa na Sh500,000, mali isiyohamishika na mmoja wapo kuwa mtumishi wa serikali au taasisi inayotambulika.


Katika kesi nyingine iliyotajwa kwa mara ya pili, Mwakalebela anadaiwa kutoa hongo ya Sh100,000 kwa Mwenyekiti wa CCM kijiji cha Mkoga, Hamis Luhanga ili awagawie wajumbe 30 waliohudhuria kikao alichoitisha.


Akisoma shitaka hayo mbele ya hakimu, mahakama ya Mkoa wa Iringa, Festo Lwelu, waendesha mashtaka wa Takukuru, Prisca Mpeka na Imani Mizizi walisema Juni 20 mshitakiwa Mwakalebela anadaiwa kutoa hongo ya sh. 100,000 kwa Hamis Luhanga ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha Mkoga ili awagawie wajumbe wa CCM 30 ambao waliitwa kwenye kikao.


Mshitakiwa alikana shitaka na aliachiwa kwa dhamana baada ya wadhamini wake wawili kutimiza masharti yote yakiwemo ya kuwa na Sh5m, kutoa ahadi ya sh5m na mmoja kuwa mtumishi wa Serikali au taasisi inayotambulika.


Mpeka alisema mshitakiwa anadaiwa kutoa rushwa kinyume cha sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) kinachokwenda sambamba na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka mwaka 2010 kifungu namba 21 (1) (a) na kifungu cha 24(8).


Frederick Mwakalebela akiwa mahakani leo.Wakazi wa Manispaa ya Iringa wakiwa wamefurika nje ya Mahakama baada ya kutoka kusikiliza kasi ya Mwakalebela leo 
Kesi zote mbili zimeahirishwa mpaka Septemba 15 zitakaposikilizwa tena. Mwakalebela anatetewa na wakili Mkwata kutoka Mkwata Law Chamber.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...