Skip to main content

MWAKALEBELA.................1

Bw. Fredrick Mwakalebela (Kulia) akiwa na Mkewe Bi. Selina Mwakalebela wakati wa mkutano na waandishi wa habari mijini Iringa jana.




FREDERICK Mwakalebela mmoja wa wanaCCM anayetafuta ridhaa ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania ubunge jimbo la Iringa Mjini amekanusha vikali madai ya rushwa yaliyotolewa dhidi yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).



Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Mwakalebela alisema hajawahi kukamatwa kwa madai hayo, lakini akakiri kuhojiwa na Takukuru ili atoe ufafanuzi kuhusu taarifa zilizotolewa dhidi yake kwa taasisi hiyo.



Akinukuu taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Iringa, Donasian Kessy kwamba Julai 20 katika kijiji cha Mgongo aliitisha kikao nyumbani kwa Gwido Sanga ambacho kilihudhuriwa na wana CCM 22, Mwakalebela alisema alikutana na wana CCM hao na kutangaza nia yake ya kuwania ubunge katika jimbo hilo, na kwamba katika kikao hicho hakutoa rushwa ya aina yoyote kama ilivyodaiwa.



"Nilikutana kweli na wanachama hao nikawaleza historia yangu, na nikatangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo hili la Iringa Mjini na baadaye nikawaleleza malengo yangu endapo azma yangu hiyo itafanikiwa,baada ya hapo nikaondoka" alisema.



Hata hivyo alisema katika mkutano huo, mkewe Selina Mwakalebela anatuhumiwa na Takukuru kwa kutoa sh 100,000 kwa wanachama hao.



"Sifahamu chochote kuhusiana na madai ya mke wangu kutoa kiasi hicho cha fedha kwa wanachama hao, na malengo ya kufanya hivyo," alisema.



Alisema anashangaa kwanini Takukuru wamemuhusisha katika madai hayo ya mkewe kutoa kiasi hicho cha fedha, hususani katika kipindi hiki ambacho wanaCCM wanaenda kufanya maamuzi magumu ya kumpata mgombea wao.



"Mke wangu ni mke wangu, lakini kama kuna ushahidi wa yeye kufanya kosa, hilo lisichukuliwe kosa la familia," alisema.



Katika taarifa yake aliyoitoa juzi kwa waandishi wa habari Kessy alisema pamoja na Mwakalebela, aliyekuwa waziri katika serikali za awamu karibu zote Joseph Mungai anayewania ubunge Mufindi Kaskazini na Mkuu wa Wilaya ya Hai, Dk Norman Sigalla anayetafuta ridhaa hiyo jimbo la Makete na Fadhili Ngajilo jimbo la Iringa Mjini,walihojiwa kwa madai ya kuhusishwa na vitendo vya rushwa katika majimbo wanayogombea.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...