Skip to main content

…VIGOGO………….1







ALIYEKUWA mshindi wa pili katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Njombe Kaskazini, Alatanga Nyagawa huenda akatimkia CHADEMA ikiwa ni hatua mojawapo ya kupinga maamuzi ya vikao vya juu vya chama hicho yaliyomteua Deo Sanga (Jah People) kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo.






Katika kura hizo, Jah people alipata kura 6,313 dhidi ya kura 2,313 alizopata Nyagawa huku mbunge mkongwe aliyemaliza muda wake Jackson Makweta akipata kura 1,671.






Akizungumza kwa njia ya simu jana, Nyagawa alisema yeye pamoja na wanaCCM wengine 11 waliokuwa wakiwania kushinda kura za maoni za jimbo hilo, walipinga matokeo yaliyompa ushindi Jah People kwa madai kwamba yalitawaliwa na mazingira ya hila na rushwa.






Nyagawa alisema tofauti na matarajio yake vikao vya juu vya CCM vimetupilia malalamiko yao ambayo yana ushahidi wa kutosha.






Nyagawa alisema kutokana na kasoro hizo hayuko tayari kuunga mkono ushindi na uteuzi wa Jah People kuwania ubunge katika jimbo hilo.






Alipoulizwa wapi hatma yake ya kisiasa itakuwa baada ya malalamiko yao dhidi ya Sanga kutupiliwa mbali, Nyagawa alisema anaendelea kupokea ushauri kutoka kwa wanaCCM na wapiga kura wengine wa jimbo hilo la Njombe.






Hata hivyo vyanzo vyetu vya habari kutoka katika jimbo hilo vimethibitisha kwamba baadhi ya wanaCCM wanaendelea na jitihada kumshawishi Nyagawa agombee jimbo hilo kwa kupitia Chadema.






Mmoja kati ya vyanzo hivyo alilidokeza gazeti hili kwamba maoni ya haraka yanaendelea kukusanywa kutoka katika kata zote za jimbo hili ili kupata ushauri zaidi kuhusiana na ushawishi huo wa kumtaka Nyagawa agombee kwa chama hicho.


Wakati hali ya kisiasa katika jimbo hilo ikiwa na mtazamo huo, wapiga kura wa jimbo la Njombe Magharibi nao wamesema wanataka sauti zao zisikike katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu na hivyo kwa hamu kubwa wanasubiri kujua hatma ya kisiasa ya aliyekuwa mshindi wa kura za maoni za chama hicho, Thomas Nyimbo.






Licha ya kuongoza katika kura za maoni Nyimbo na mbunge aliyemaliza muda wake Yono Kevela ambaye katika kinyang’anyiro hicho alishika nafasi ya pili, NEC iliwatupilia mbali na nafasi ya kuliwania jimbo hilo ilikwenda kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (Tanroads) mkoa wa Dodoma, Greyson Lwenge.






Katika kura hizo Nyimbo alipata kura 6,795 dhidi ya kura 3,434 alizopata Kevela na 2,971 alizopata Lwenge katika kinyang’anyiro hicho kilichokuwa na wagombea 13

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...