Skip to main content

VIKAO VYA MAHAKAMA RUFANI





OFISI ya Mkurugenzi mkuu wa mashitaka nchini (DPP), imeiondoa rmahakamani rufaa iliyokata kwenye mahakama ya rufaa ya Tanzania, dhidi ya Philbert Mtweve aliyeomba rushwa ya sh. 15,000 kwa mwalimu wa Shule ya Msingi Kennedy Rubindu.


Wakili wa serikali, Vicent Tangoh, aliomba kuondoa rufaa hiyo kupitia kanuni ya 4(ii)(a) ya mwaka 2009 ya mahakama ya rufaa, mbele ya majaji watatu waliokuwa wakisikiliza rufaa hiyo, Edward Rutakangwa, Natalia Kimaro na William Mandia.


"Awali tuliwasilisha taarifa ya kuondoa rufaa hii kwa kanuni ya 77(i) na tukagundua kanuni hiyo sio sahihi kuitumia kwani inaeleza kuondoa rufaa kwa msajili na sio mahakama ya rufaa, hivyo sasa tunaomba kwa kupitia kanuni ya rufaa kuondoa rufaa hii," Tangoh aliwaeleza majaji hao mahakamani hapo.


Baada ya ombi hilo, Jaji Rutakangwa alishauriana na wenzake na kukubaliana na ombi hilo na kuamua kuondoa rufaa hiyo iliyokuwa imekatwa na DPP.


Awali mwaka 2001, Mtweve alidaiwa na mahakama ya Wilaya ya Mbinga kuwa alichukua rushwa ya sh. 15,000 kutoka kwa Rubindu aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi ili amsaidie kumhamishia katika shule ya maeneo ya karibu na wazazi wake.


Hata hivyo, mahakama hiyo ilimuachia huru Mtweve baada ya kukosekana ushahidi lakini serikali kupitia makahama kuu walikata rufaa na Jaji Manento alitoa uamuzi mwaka 2002 wa kuona mshtakiwa hana hatia na baadaye DPP tena akakata rufaa kwenye mahakama ya rufaa Tanzania kupinga maamuzi hayo, lakini mwanasheria wake ameondoa rufaa hiyo mahakamani.


Wakati huohuo,Rufaa ya Yassin Thomas wa Songea ya kupinga kunyongwa hadi kufa iliyotolewa mwaka 2007 baada ya kumuua Mwanaidi Abdallah mwaka 2004, iliyokuwa isikilizwe leo kwenye mahakama ya rufaa ya Tanzania iliyoketi Iringa imesogezwa mbele hadi Ijumaa (Agosti 20), baada ya wakili wa kujitegemea, Basil Mkwata kuomba ili aweze kupitia sababu za rufani hiyo.


"Mwenyekiti, nilikuwa Dodoma katika kikao cha nusu mwaka cha mawakili na nikiwa njiani kurudi nikaambiwa nipitie hapa kuna rufaa na sijapata muda wa kupitia faili la kesi hii, naomba ipangwe siku nyingine ili niweze kusoma sababu za rufaa," aliomba Mkwata kwa Mwenyekiti wa jopo hilo la majaji.


Hatahivyo wakili wa serikali Michael Lwena alipendekeza isikilizwe Agosti 27, lakini Jaji Rutakangwa baada ya kujadiliana na wenzake walipanga kuwa Ijumaa, huku akimtaka wakili huyo kuhakikisha anasoma sababu hizo kwani ameahirisha kwa shingo upande kutokana na mahakama hiyo kuwa na rufaa nyingi zisizotoa muda wa mapumziko.


Mahakama hiyo iliyoanza jana inajumla ya rufaa 30 ambazo za jinai ni 24 na zilizobaki ni za madai na inatarajiwa kumalizika Septemba 6.
MWISHO
*****





UPUNGUFU wa majaji wa mahakama ya rufaa ya Tanzania unasababisha rufaa nyingi kuchukua muda mrefu kusikilizwa na kutolewa maamuzi, imeelezwa.


Naibu Msaijili wa mahakama ya Rufaa Tanzania, John Mgetta alibainisha hayo leo mara baada ya kikao cha kusikilizwa rufaa zilizokatwa na pande mbalimbali wakipinga maamuzi ya mahakama kuu, kilichokaa Iringa na kujumuisha pia rufaa za Songea.


Mgetta alisema majaji hao wapo 16 pekee ambapo wanatakiwa kujigawa katika kanda 10 huku Dar es Salaam ikiwa na majaji sita tofauti na kanda nyingine ambao ni watatu pekee.


Alisema majaji hao 16 wanatakiwa kutoa maamuzi katika kanda za Arusha, Dodoma, Tanga, Mbeya, Sumbawanga, Mwanza, Tabora, Mtwara, Dar es Salaam na Iringa.


Alitoa mfano wa Kanda Iringa inayokaa mara moja kwa mwaka ikijumuisha rufaa za Iringa na Songea rufaa zake zimeanza jana ambazo zipo 30 na zinasikilizwa na majaji watatu, Edward Rutakangwa, Natalia Kimaro na William Mandia na zitamalizika Septemba 6.


"Angalia mtu kakata rufaa tangu mwaka 2008 mwaka huu ndo inaanza kusikilizwa na hii ni sababu ya majaji wachache kwani kama wangekuwa wengi ingekuwa imeshaisha," alisema Mgetta.
MWISHO
*****





































Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...