Skip to main content

WAGOMBEA WAREJESHA FOMU ZA UTEUZI

WAGOMBEA ubunge katika majimbo ya Iringa mjini, Kalenga na Ismani mkoani Iringa warejesha fomu za uteuzi katika ofisi ya tume ya uchaguzi za Iringa Mjini na Iringa Vijijini leo.


Katika Jimbo la Ismani, ni mgombea mmoja tu ambaye ni Bw. William Lukuvi (CCM) ndiye karudisha fomu ya uteuzi kati ya wagombea watatu waliochukuwa fomu pamoja na Bw. Joseph Kapwani (CHADEMA) na Bw. Juma Fufumbe (CUF).


Bw. Lukuvi atatangazwa mshindi wa bila kupingwa katika Jimbo la Isimani baada ya maasa 24 na Msimamizi wa Uchaguzi, Bi. Tina Sekambo wa Wilaya ya Iringa, baada ya wagombea wengine kutorudisha fomu zao kabla ya saa 10 jioni.


Katika Jimbo la Kalenga, waliochukuwa fomu walikuwa wanne na wote wamerudisha fomu zao kabla ya muda uliopangwa na tume ya uchaguzi (NEC).


Waliochukuwa fomu za uteuzi na kurejesha ni pamoja na Bw. Katindasa Lumunko (TLP), Dkt. William Mgimwa (CCM), Bw. Makuke Majinga (Jahazi Asilia)na Bi. Rehema Paulo (CHADEMA).


Katika jimbo la Iringa Mjini ambapo aliyekuwa mshindi katika kura za maoni mwanzoni mwa mwezi huu, Bw. Frederick Mwakalebela ambaye pia ayeeuenguliwa NEC ya chama cha CCM baada ya kashfa ya kutoa rushwa na kesi yake inaendelea mahamani, na kumteuwa mshindi wa pili Bi. Monica Mbega kupitia tiketi ya CCM, basi urejeshaji wa fomu za uteuzi za ubunge umekamilika vizuri leo.


Bw. Willam Lukuvi akiongea na wana habari leo baada ya Msimamizi wa Uchaguzi katika Wilaya ya Iringa Bi. Tina Sekambo kumaliza kubandika fomu za uteuzi ubaoni.Mchungaji Peter Msigwa akirudisha fomu ya uteuzi leo kwa msafara wa gari mjini Iringa.
Waliochuwa na kurudisha fomu katika jimbo la Iringa mjini ni pamoja na Bi. Monica Mbega (CCM), Bi. Mariam Mwakingwa (NCCR-Mageuzi), Bi. Zaituni Mwaibula (CUF) na Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA).



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...