Skip to main content

WALIMU WAKOPESHWA PIKIPIKI

Pikipiki zikiwa nje ya ofisi ya SACCOS ya walimu mjini Iringa.

Na Friday Simbaya,
Iringa

CHAMA cha Ushirika cha Akiba na Kukopa cha Walimu wa Iringa Vijini na Kilolo (IRTS-SACCOS LTD) kimekabidhi pikipiki kwa walimu wanachama 19 katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya chama hicho jana.

Pikipiki hizo 19, zilitolewa kwa walimu 19 kati ya 27 walikubaliwa kupewa na juhudi zaidi zinafanyika kupata pikipiki nyingine nane (8) zilizobaki ili walimu hao nao waweze kupewa mapema.

Akikabidhi pikipiki kwa walimu, Afisa Elimu wa Wilaya shule za msingi (DEO), William Mkagwa, kwa niaba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Iringa (DED), Tina Sekambo, alisema kuwa amefurahishwa na juhudi za SACCOS ya kutatua matatizo ya usafari kwa walimu wanachama kwa kutoa mikopo ya pikipiki ambazo zitarahisisha sana usafari kutokana na hali ya jiografia ya Wilaya.

Aidha, Sekambo alishauri pia utaratibu wa mikopo ya vyombo hivi uwe endelevu ili hatimaye walimu wote waweze kupata vyombo hivi.

“Ningependa pia nizungumza suala la mikopo, wafanyakazi wengi wamekuwa na tabia ya kukopa katika taasisi mbalimbali zaidi ya mkopo mmoja kwa wakati, ni vizuri ukamaliza mkopo huu wa pikipiki kabla ya kukopa kwingine, kwani mwisho wa siku familia itapata maisha magumu sana pale mfanyakazi anapokuwa hana cha kupeleka nyumbani mwisho wa mwezi,” alisema.

Aliongeza kuwa vyombo hivi vikitumiwe vizuri kwa sababu vinaweza kuwa kichocheo cha kuinua taaluma na maisha ya walimu katika wilaya.

Lakini vyombo hivyo vya usafari vikitumika vibaya vinaweza kuleta madhara makubwa kwa walimu na hatimaye kurudisha nyuma juhudi za wizara katika kutoa elimu bora kwa watoto na kubadilisha maisha ya walimu.

Katibu wa SACCOS, John Mfalamagoha alisema kuwa chama kilianzishwa mwaka 1997 hadi kufikia tarehe 30/07/2010 chama kilikuwa na jumla ya wanachama 1,197 kati yao wanaume ni 564 na wanawake ni 633.

Alisema kuwa walimu waliomba mkopo ni 27 wakiwamo wanaume 20 na wanwake saba (7) lakini walikabidhiwa ni wanaume 12 na wanawake saba jumla 19, na utaratibu wa kupata pikipiki zilizobaki unaendelea kufanyika na zikipatikana wakati wowote zitakabidhiwa kwa waliomba.

Aidha, katibu huyo alisema, malengo ya chama yalikuwa kutoa mkopo wa pikipiki 50 kwa mwaka 2010 lakini waombaji hawakujitokeza kwa wengi na hivyo kufanikiwa kupata waombaji waliokabidhiwa pikipiki jana.

Takwimu zinaonyesha kuwa watu waliopoteza maisha kutokana na ajali za pikipiki nchini mwaka 2010 181 kati ya jumla ya ajali 1,414 zilizotokea. Pia takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 16 ya ajali ya 30,836 za ajali zilizotokea mwaka 2009.

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...