Skip to main content

WAPAMBE WA MBUNGE LUDEWA WACHANA KADI ZA CHAMA

Moja za kadi za chama zilizochanwa na wapambe wa mbunge Prof. Rapheal Mwalyosi huko Ludewa hivi karibuni.


WANA Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani Ludewa wamesikitishwa na kitendo kilichofanywa na wapambe wa mbunge wa zamani wa Jimbo la Ludewa (CCM) Prof. Raphael Mwalyosi kuchukua kadi zao na kuzichana .
Wapambe hao wanaodaiwa kuchukua kadi za wana CCM na kuzichana ni Boscow Thobias Lingala Lingala,Obote Msemakweli, Aulerian Mhagama (Amca) na Florian Mtweve (Mvanginye) huku kadi za wana CCM hao zilizochanwa ni zile za kata za Ludewa Mjini, Manda na Nkomang’ombe ambao walikuwa wakimpinga Mwalyosi na kumuunga mkono Filikunjombe.
Siku mbili kabla ya kura za maoni wapambe wa Prof. Mwalyosi walikuwa wakienda kwenye zile Kata asizokubalika Profesa wakinunua kadi moja ya CCM kwa shilingi 10,000/= mpaka 20,000/= toka kwa wana CCM na kuzichana ili kuwafanya wanachama hao wasipige kura wakihofia kuwa wakifanya hivyo watawapigia wagombea wengine.
Wakati kadi zilizochanwa Manda zilitupwa chooni kadi zilizochanwa Ludewa Mjini zilitupwa kwenye jalala la kilabu cha Pombe za Kienyeji cha Henry kilichopo Ludewa Mjini.
Blog hii imeviona vipande vipande vya kadi za CCM viingine vikiwa vimeunguzwa na moto jalalani hapo na vingine vikiwa vimetapakaa pembeni ya jalala hilo.
Wagombea wengine walioshiriki kwenye mchakato wa kura za maoni Jimboni Ludewa ni Injinia Zebadiah Chaula, Deo Filikunjombe – Kamanda wa Vijana UVCCM (W) na James Mgaya.
Allen Ngingo, Katibu Kata wa Kata ya Ludewa Mjini ambako kadi za CCM pia zilichanwa amelaani kitendo kilichofanywa na Mbunge huyo wa zamani (Prof. Mwaloysi).
“Hatukutegemea kama Profesa anaweza kuchana kadi za Chama kilichomweka madarakani kwa miaka mitano,” alilalamika Katibu Kata huyo akiongeza kuwa “Sisi tumekitafsiri kitendo hicho kama ni mbinu mahsusi za kutaka kukihujumu Chama Cha Mapinduzi, kwa maslahi binafsi.”
Lakini pia sisi tumesikitishwa zaidi kuona kuwa baadhi ya walioshiriki kuzichana kadi hizo za CCM ni watumishi wa serikali,” alisema kwa uchungu mwana CCM mwingine mkongwe, Andrew Nyilawila, 75. “Sielewi kabisa; mtumishi wa serikali anawezaje kuchana kadi ya chama tawala?” alihoji Bw. Nyilawila.
Katibu wa CCM wa Wilaya ya Ludewa, Mama Magreth Chusi, amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kusema kuwa swala hilo linashughulikiwa kiChama ndani ya CCM na kwamba hatua stahiki zitachukuliwa kwa waliofanya hivyo. “Tumelifikisha swala hilo kwenye vyombo husika,” alisema mama Chusi.
Katibu wa Mkoa wa Iringa, Mary Tesha naye amekiri kuzipokea taarifa za kuchanwa chanwa kwa kadi za CCM jimboni Ludewa.
“Taarifa ambazo nimezipata zimenistua na zimenisonesha sana,” alisema Mary Tesha huku akiongeza kuwa uchunguzi makini unaendelea ili kuwabaini wale waliohusika na vitendo hivyo na kwamba hatua kali zitachukuliwa kwa watakao bainika kuihujumu CCM.
Hata hivyo Prof.Mwalyosi mwenyewe hakuweza kupatikana katika simu yake ili kujibia madai hayo dhidi yake .
Prof. Raphael Mwalyosi alikuwa Mbunge wa Jimbo la Ludewa (CCM) toka mwaka 2005 hadi 2010 amedondoshwa kwenye kura za maoni na mwandishi wa habari, Bw. Deo Filikunjombe aliyepata ushindi wa kura 7175 huku Prof. Mwalyosi Raphael (6,652),James Mgaya (588) na Chaula Daniel (461).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...