Skip to main content

KAPWANI ASIMAMISHWA UENYEKITI

KAIMU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bw. John Mnyika, amempa siku 14 aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Isimani mkoani Iringa, Bw. Ben Kwapwani kutoa utetezi wake kwa maandishi kabla ya chama hicho hakitaja mwajibisha kwa kukikuka katiba ya Chadema.


Mbali na agizo hilo, pia Bw. Kapwani amesimamishwa rasmi nafasi ya Uenyekiti wa Mkoa wa Chama hicho hadi hapo uongozi wa juu utakapojiridhisha kuhusiana na shutuma mbalimbali zinazomkabili kada huyo.


Kwa mujibu wa barua ya Mnyika ya Septemba 14 mwaka huu aliyomwandikia Kapwani, ikiwa na kumbukumbu namba C.HQ/ADM/M/IR/05 inaeleza kuwa miongoni mwa mambo anayotakiwa kutolea maelezo ni pamoja na kushindwa kurudisha fomu ya uteuzi ya kugombea ubunge katika Jimbo la Isimani.


Shutuma nyingine zinazotakiwa kutolewa maelezo ni kuonekana kwake machoni pa umma akimnadi mgombea wa chama kingine wakati Chadema imesimamisha mgombea wake wa ubunge Iringa mjini ambaye anakubalika na wananchi wengi.


Anadaiwa kumpigia debe hadharani mgombea ubunge wa NCCR-Mageuzi Mariam Mwakingwe ambaye pia anaungwa mkono na muungano wa vyama vya upinzani vya TLP,DP,UDP na Chausta.


“Masuala hayo ni kinyume cha maadili ya chama kifungu cha 10.1 (viii),(xii) na 10.2 (10),(xi) zenye kutoa maadili ya viongozi na sifa mahususi za viongozi kwa pamoja.


Hata hivyo,Kwapani aliliambia mwandishi kwa njia ya simu jana kuwa yeye hajapokea barua hiyo hadi sasa lakini akadai haukubaliani na agizo hilo kwakuwa mwenye uwezo wa kumsimamisha uenyekiti ni mkutano mkuu wa mkoa na si Katibu mkuu kama alivyofanya Mnyika.


“ Mimi sijapata hiyo barua hadi tunavyoongea lakini hata hivyo huyo Mnyika au Katibu mkuu wa Chadema Dk. Wilbrodi Slaa hawezi kunisimamisha Uenyekiti isipokuwa mkutano mkuu pekee….Lazima aelewe mimi siwajibiki kwake”,alisema Kapwani.


Kuhusu tetesi kwamba leo Kapwani alikuwa akimsubiri mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Jakaya Kikwete ili ajiunge na Chama hicho katika uwanja wa Samora mjini hapa,Kapwani alisema si kweli kama jinsi ambavyo inadaiwa ila yeye bado ni mwana Chadema na ataendelea kukitumikia chama chake.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...