Skip to main content

PINGAMIZI LA MUNGAI LA KWAA KISIKI KWA MARA NYINGINE

PINGAMIZI la awali la kutaka kuondolewa mahakamani kesi ya kutoa hongo katika mchakato wa kura za maoni, inayomkabili aliyewahi kuwa Waziri katika serikali za awamu zote nne, Joseph Mungai (66), imeshindwa kuanza kusikilizwa baada ya upande wa mashitaka (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa), kuomba pingamizi hilo liwasilishwe mahakamani kwa njia ya maandishi.


Mungai pamoja na makada wengine wawili wa CCM, akiwemo Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Mufindi, Fidel Cholela (39) na Moses Masasi wanakabiliwa na mashtaka 15 ya kutoa rushwa kinyume na sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa ya mwaka 2007 na sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010.


Mawakili wanaomtetea Mungai,aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini (CCM), Alex Mgongolwa na Basil Mkwata, LEO walifika katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa, kuwasilisha pingamizi hilo kwa lengo la kuanza kusikilizwa.


Wakiwa mbele ya hakimu anayesikiliza kesi hiyo namba 5 ya mwaka 2010, Mary Senapee, mawakili hao waliiomba mahakama hiyo kuruhusu pingamizi hilo kuwasilishwa na kuanza kusikilizwa kama ilivyopangwa, kwakuwa kesi hiyo ina mvuto kwa jamii.


“ Mheshimiwa, kesi hii kama unavyoiona ina public interest, hivyo kama itaendeshwa kwa njia ya maandishi, umma hautaweza kufahamu maendeleo ya shauri lenyewe linavyokwenda”alisema mmoja wa mawakili wa Mungai, Basil Mkwata huku,


Wakili Alex Mgongolwa, akiieleza mahakama hiyo kuwa pingamizi zinazowasilishwa mahakamani hapo zinatokana na maandalizi ya kesi hiyo ya Takuku na kwamba hakuna kitu kipya, hivyo ni vyema upande wa mashitaka , wakajipa nafasi ya kusikiliza pingamizi hizo ni zipi badala ya kutaka kuchelewesha kusikilizwa kwa shauri hilo kwa kuomba upande wa utetezi tuwasilishe pingamizi kwa njia ya maandishi.


Awali, mwendesha mashitaka wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Iringa (Takukuru), Bw. Imani Nitume aliiomba mahakama hiyo, kuamuru upande wa utetezi uwasilishe pingamizi hilo mahakamani hapo kwa njia ya maandishi na si kama ilivyokusudia kuliwasilisha kwa njia ya kawaida (Oral) na kutaka ianze kusikilizwa.


“Mheshimiwa,tunakuomba kama ikikupendeza tupate pingamizi hili kwa njia ya maandishi, sipingani na hoja iliyotolewa na upande wa utetezi kwamba shauri hili lina public interest lakini bado upande wa mashitaka tunasisitiza wawasilishe pingamizi kwa njia ya maandishi… kwakuwa kesi hii inahitaji umakini mkubwa katika kusikiliza na kuiendesha ”, alisema mwendesha mashitaka huyo wa Takukuru.


Baada ya mabishano ya muda mrefu ya kisheria, hakimu Mary Senapee alisema anakubaliana na hoja za pande zote mbili lakini hoja hizo haziwezi kuzuia mahakama hiyo kuendelea na hivyo akakubaliana na ombi la upande wa mashitaka katika shauri hilo kwamba pingamizi hilo liwasilishe kwa njia ya maandishi.


Mfululizo wa mabishano ya hoja hizo za kisheria, uliishia kwa upande wa utetezi kukubaliana na mahakama hiyo kuwasilisha pingamizi lao Oktoba 22 mwaka huu, huku upande wa mashitaka nao ukiiomba mahakama hiyo ya hakimu mkazi Mkoa wa Iringa, nao wajibu pingamizi hilo Novemba 05 mwaka huu.


Baada ya ombi hilo Hakimu Senapee alisema shauri hilo litafikishwa tena mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa Novemba 12 mwaka huu kwa ajili ya kupanga tarehe ya kuanza kusikilizwa kwa pingamizi hilo.


Inadaiwa kuwa Julai 08, mwaka huu, katika kata ya Ihalimba, Wilaya ya Mufindi, Mungai akiwa mmoja wa makada wa CCM waliokuwa wanawania kupitishwa katika kura za maoni kugombea ubunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, kwa pamoja na watuhumiwa wenzake, walitoa hongo ya Sh.10,000 kwa Mwenyekiti wa CCM tawi la Vikula kama kishawishi cha kumpigia kura wakati wa zoezi la upigaji wa kura za maoni.


Katika shitaka la pili, inadaiwa kuwa watuhumiwa wote kwa pamoja, siku na katika eneo hilo walitoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Konjesta Kiyeyeu ambaye alihudhuria kikao cha kamati ya CCM Kijiji cha Vikula.


Katika shtaka la tatu, nne, tano na sita, watuhumiwa wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Aldo Lugusi, Ezekiel Mhewa, Tulaigwa Kisinda na Jiston Mhagama kwa lengo hilo hilo la kuwashawishi wampigie kura za maoni.


Katika shitaka la saba,watuhumiwa hao wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.20,000/- kwa Maria Kihongosi na shtaka la nane kutoa hongo ya Sh.5,000/- kwa Lurent Mdalingwa wakati shtaka la tisa wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.20,000/- kwa Victory Kalinga ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Kijiji cha Ugessa.


Katika mashtaka namba kumi hadi 12 washtakiwa wote kwa pamoja wanadaiwa walitoa hongo ya Sh.2,000/- kwa Francis Chonya, Alfred Kisinga na Issac Tewele wakati shtaka la 13 wanadaiwa walitoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Sosten Kigahe.


Mashitaka mengine, namba 14 watuhumiwa wanadaiwa kutoa hongo ya Sh.10,000/- kwa Raphael Lutumo na shitaka la mwisho walitoa hongo ya Sh.20,000/- kwa Andrew Mkiwa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...