Skip to main content

CHAVITA YAOMBA SERIKALI KUBORESHA MAISHA YA WALEMAVU

CHAMA cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Mkoa wa Iringa chaiomba serikali kuboresha mazingira na maisha ya watu wenye ulemavu nchini za kupata huduma za elimu, afya na usalama wa raia kama watu wengine.



Mwenyekiti wa CHAVITA Mkoa wa Iringa Zawadi Sumani alisema jana katika warsha ya ushawishi na utetezi kwa watendaji wa idara za serikali na viongozi wa serikali za mitaa Mkoa wa Iringa, kuwa watu wenye ulemavu ni waathirika wakubwa wa umaskini na UKIMWI hapa nchini kutokana na mitazamo potofu ya jamii inayoizunguka.


Alisema kuwa huduma na sheria mbalimbalinzilizopo hapa nchini hazikidhi maitaji ya watu wenye ulemavu na wemekuwa wakiacwa nyuma katika mchakato mzima wa maendeleo ya taifa ingawa zipo jitihada mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanywa na serikali katika kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanapata huduma za elimu, afya na usalama wa raia.


Lakini bado inaelekeza dhana kuwa mtu mwenye ulemavu anastahili kuishi maisha tegemezi ambapo dhana hii ina kwenda kinyume na tamko la umoja wa mataifa kuhusu haki za binadamu na azimio kuhusu fursa sawa na ushirikishaji wa watu wenye ulemavu la mwaka 1983.


Lengo mahususi la warsha iyo ilikuwa ni kuwapatia mwako watendaji kutoka idara mbalimbali kama polisi watendaji wa mahospitali na uongozi wa serikali za mitaa kutoka ngazi ya Mkoa hadi wilaya kutambua umuhimu wa ushiriki wao katika kufanyikisha mchakato wa uimarishaji wa sera na sheria za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya mtaa, kata, tarafa hadi wilaya.


Aidha, alisema kuwa serikali hivi sasa inatekeleza awamu ya pili ya mpango wa miaka mine wa kuondoa umaskini, maarufu kama mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini (MKUKUTA, mpango huu pamoja na mambo mengine unatambua wenye ulemavu.


Warsha ya utetezi na ushawishi kwa watendaji idara mbalimbali uliaandaliwa na CHAVITA kwa kushirikiana na shirika la ‘The Foundation for Civil Society’ kwa kutoa ruzuku ambayo imefanyikisha uendashaji wa warsha ya siku nne.


Mkoa wa Iringa una kadiriwa kuwa na idadi ya walemavu wasiosikia yaani viziwi zaidi ya 2,000 wanaotabulika na chama cha viziwi Tanzania Mkoa wa Iringa.


Kwa upande wake, Mgeni Rasmi Kaimu Mkuu Mkoa wa Iringa Kapteni mstaafu Aseri Msangi, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa alisema serikali ipo bega kwa bega kuhakikisha watu wenye ulemavu hasa viziwi wanaendelea kuimarishwa kwa misingi ya kuboresha hali za maisha yao.


Alisema kuwa Chama cha tawala (CCM) kwa kuboresha ilani ya uchaguzi imeangalia mahitaji ya watu wenye ulemavu kwa kuwawekea mikakati mabalimbali ya maendeleo ya taifa, mikakati hii itasaidia sana katika kuwakomboa watu wenye ulemavu kwenye umaskini na majanga mbalimbali yanayokithiri miongoni mwa jamii ya watu wenye ulemavu hapa nchini.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kapteni (mstaafu) Aseri Msingi mwenye Kaunda suti ya bluu  kutoka kushoto mstali wa mbele ya watu walioketi akiwa katika picha ya pamoja ya viongozi wa Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) na washiriki wa warsha ya siku nne ya ushawishi na utetezi kwa watendaji wa idara za serikali na viongozi wa serikali za mitaa Mkoa wa Iringa jana. (PICHA. FRIDAY SIMBAYA)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...