Skip to main content

CHUO CHA PERAMIHO CHA KABILIWA NA CHANGAMOTO

Na Friday Simbaya,
Peramiho

Ijumaa ya tarehe 19 Novemba ya mwaka 2010 Chuo cha Ufundi cha Peramiho (Peramiho Vocational Training Center) kilichopo Jimbo la Songea, mkoani Ruvuma, kilifanya mahafali yake ya 79 ambapo jumla ya wahitimu 23 walitunikiwa vyeti vya kumaliza mafunzo katika fani mbalimbali.

Katika mahafali hayo jumla ya wahitimu 23 walitunukiwa vyeti vya kumaliza mafunzo katika fani ya ushonaji, ufundi magari na useremala ambapo vijana waliohitimu wanakamilisha idadi ya wahitimu jumla 1,718 katika chuo hiki tangu kuanzishwa kwake mwaka 1928.

Chuo cha ufundi Peramiho kilipata usajili kwa mujibu wa sheria za nchi kwa kuendasha mafunzo chini ya uratibu na muongozo wa VETA ambao ni waratibu wakuu wa mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania.

Mahafali hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Mtakatifu Benediktini hapa Peramiho na kuhudhulia na wageni mbalimbali kutoka taasisi mbalimbali za hapa Peramiho (Shule ya Wasichana Peramiho, Sekondari ya Sili, Sekondari Maposeni, Daraja Mbili, Chuo cha Uuguzi, Hospitali Peramiho, Seminari Kuu Peramiho na Masista Tutzing).

Awali, Mkuu wa Chuo cha Ufundi Peramiho Bro. Joseph Mukasa alitoa taarifa ya mafunzo kwa mgeni rasmi ambaye alitarajiwa kuwa ni mkurugenzi wa kanda za juu –VETA, katika Mahafali ya 79 Peramiho VTC, lakini kwa niaba yake alimuagiza Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) cha Songea Bw. Afridon Mkhomoi.

Bw. Mukasa alisema kuwa chuo chake kia jumla ya wanachuo 116 ambapo wasichana 44 na wavulana 72. Aidha, idadi ya wanachuo katika mwaka ujao (2011) itaongezeka kutoka wanafunzi 116 hadi kufikia idadi ya 160, ilikuenda sambamba na uboreshaji na uongazaji wa miundombinu hususani mabweni ya wasichana.

Alisema kuwa vijana waliyohitimu mafunzo walitoka katika fani zifuatazo: ushonaji nguo za kike na za kiume walikuwa 12(wavulana 4 wasichana 8), ufundi magari(MV Mechanics) walikuwa wavulana 6 na msichana 1 na useremala walikuwa wavulana 4 na kufanya jumla ya wahitimu wote 23.

BAADHI YA CHANGAMOTO WANAZOKABILIANA NAZO

Mahali penye mafanikio hapakosi kuwepo na changamoto, Chuo Cha Ufundi cha Peramiho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali lakini kubwa zaidi ni lile la kupungua kwa misaada kwa chuo siku hadi siku pamoja na kupanda kwa gharama ya za maisha.

Chuo hiki sasa kina umri wa miaka 82 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1928, umri huu si mdogo una changamoto zake katika uendeshaji wake wakati huu wa ulimwengu wa sayansi na teknolojia.

• Uchakavu wa miundo mbinu kama vile vitendea kazi na mitambo, ambapo kwa kiasi kikubwa imepitwa na wakati.
• Uchakavu na uchache wa nyumba za watumishi.
• Mabweni ya wasichana kwa ajili ya wasichana hayatoshi na hii inasababisha chuo kipokee idadi ndogo ya wasichana kwa ajili ya mafunzo.
• Kitengo cha komputa hakina komputa za kutosha ili kukidhi uwiano wa 1:1.

Pamoja na changamoto wazokabiliwa nazo kama chuo ipo pia mikakati waliojiwekea kwa kipindi kijacho kuanzai mwaka 2011.

1. Kuannzisha fani mpya ya Printing Press’ inayounganishwa na ‘Computer Application’.
2. Kuanshia shule ya mafunzo ya udereva kwa kozi fupi fupi (Driving School).
3. Kuendelea na zoezi la kuwajengea uwezo wakufunzi wetu kwa kuwepeleka Chuo Cha Ualimu Morogoro au Off Campus Songea.
4. Kukarabati majengo ya Mruma Center kwa ajili ya hostel ya wasichana.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika nasaha za zake Bw. Afridon Mkhomoi kwa nia ya mkurugenzi wa kanda nyanda za juu-VETA, alikipongeza chuo kwa mafaniko makubwa ya chuo hicho likiwemo swala la kutoa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana.

Alisema kuwa vjiana wakiwezeshwa wanaweza kujiajiri na kujitegemea wenyewe kwa kuanzisha miradi mbalimbali hatimaye kupunguza umasikini.

Pamoja na pongezi hizo mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA cha Songea, aliusihi uongozi wa chuo cha peramiho kuanzisha kuotoa fani ngazi ya diploma kutokana na chuo hicho kuwa kikongwe an kuwa waanzilishi wauutoaji mafunzo ya ufundi stadi nchini.

Alisema kuwa kutokana na umri wa chuo hicho kinastahili kabisa kuanzisha program za diploma.


Aidha, mkuu wa chuo cha Songea alihaidi kuwa VETA katika mwaka fedha wa bajeti ujao watasaidia Chuo Cha Peramiho katiak masuala mazima ya vifaa ilikiweza angalau kusonga mbele.

Baba Abate,[Mkuu wa shirika la wabenedictini]Abasia Peramiho, Anastasius Reizer ,ambaye ni abate wa nne tangu kuanzishwa shirika hapa Peramiho, naye ni mtu anayejali na kufuatilia kwa karibu ufanisia katika Nyanja ya elimu hapa Abasiani, kwani ndiye mfadhili mkuu kwa kukiwezesha chuo zaidi ya thelusi mbili ya gharama za uendeshaji wa chuo hicho.

Kwa kweli anatakiwa pongezi za pekee na bila kuficha ni mfano wa kuigwa na wengine.




Baba Abate Anastasius Reiser (OSB-Mkuu wa Shirika la wabeneditini )  Abasia Peramiho

Mkuu wa Chuo cha Ufundi Peramiho Br. Joseph Mukasa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake hivi karibuni.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...