Skip to main content

MAMBO YA SIASA HAYO

MWENYIKITI wa kijiji cha Nduli, Ayubu Mwenda amedai kuwa Diwani wa kata mpya ya Nduli iliyopo Manispaa ya Iringa amekuwa akimtishia kumwondoa madarakani na pia kumnyang’anya ardhi na kuikabidhi kwa serikali ya kijiji kutokana na chuki za kisiasa.



Chuki zilizotokana na wote kuomba kuteuliwa katika kura za maoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania nafasi ya Udiwani kwenye kata hiyo ambapo mwenyekiti huyo hakubahatika kupata nafasi na kukata rufaa ya kupinga matokeo ya kura za maoni lakini rufaa yake ilikataliwa na Idd Chonanga kupita kuwania udiwani.


Mwenda amedai kuwa vitisho hivyo alianza kuvitoa mara baada ya kupita kwenye kura za maoni pamoja na kwenye kampeni ya kujinadi kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu (Oktoba 31, 2010).


“Pamoja na kuwa kampeni meneja wa CCM wa kata ya Nduli lakini nimeonekana kuwa mpinzani kwake kwani alihisi kutokana na kushindwa kwangu ningesaidia vyama vya upinzani dhana ambayo si kweli kwa kuwa mimi ni kada wa CCM” alisema Mwenda.


Alisema mbali na yeye kupata vitisho vya kuondolewa madarakani mara baada ya kupita kwenye kinyang’anyiro cha Udiwani, diwani huyo pia alisema atahakikisha eneo analolimiliki linalokadiriwa kuwa na ekari 60 kumnyang’anya na kulikabidhi serikali ya kijiji ili lijengwe sekondari ya kata kwa lengo la kumkomesha.


“Eneo hilo lilikuwa mali ya baba yangu mzazi Abdallah Athumani Mwenda……..ambalo awali kabla ya kumiliki baba lilikuwa mashamba ya Wagiriki ambalo walikuwa akilima tumbaku na baadaye wagiriki kuondoka na kumwachia baba ambaye alikuwa akifanya kazi kwao” alisema mweyekiti huyo wa kijiji cha Nduli.


Kwa upande wake Diwani wa kata ya Nduli, Idd Chonanga alidai tuhuma hizo alizozitoa mwenyekiti huyo si za kweli hajawahi kusema labda ni kwa vile walikuwa wakichuana katika kura za maoni za CCM hivyo anahisi atamfanyia hivyo.


“Serikali ya kijiji ndiyo yenye mamlaka ya kumnyang’anya mkazi ardhi na kuimiliki na kuamua eneoe hilo litumike kwa shughuli zipi, hivyo mimi siwezi kumnyang’anya eneo hilo ” alisema Diwani Chonanga.


Aidha kwa upande wake Mohamed Mwenda (kaka yake Ayubu) alidai kuwa hajawahi kusikia eneo hilo kutaka kuchukuliwa na kukabidhiwa kwa serikali ya kijiji na kudai kuwa eneo hilo lenye jumla ya ekari 159 lilimilikishwa kwa mjukuu wa baba aitwae Ahamadi Mzola kwa kushirikiana na mimi (Mohamed Mwenda) kupitia wosia aliouandika Abdallah Athumani Mwenda.


Naye Afisa mtendaji wa kata ya Nduli, Hamid Mfalingundi alisema anamshangaa mwenyekiti huyo kwa kudai kunyang’anywa eneo ili lijengwe sekondari ya kata mbali na kufahamu kuwa tayari kikao kilishaamua eneo la kujenga sekondari ya kata na yeye alishiriki katika kikao hicho.


Mfalingulindi alisema makubaliano ya kujenga sekondari kwenye kikao hicho yalikuwa ni kitongoji cha Kisowele ambacho kipo kati kati ya kijiji cha Mgongo, Nduli na Kigonzile.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...