Skip to main content

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete afanye maamuzi magumu na mazito katika uteuzi wa waziri mkuu wa serikali ya Tanzania kwa kipindi chake cha mwisho cha urais kwa mujibu wa katiba ya CCM.


Kama ilivyofanyika maamuzi magumu ya kumuondoa spika wa bunge lililopita Mh. Samuel Sitta na hatimaye Mh. Anna Makinda kuwa spika wa kwanza mwanamke katika historia ya Tanzania. Huu ulikuwa uamuzi mgumu na mzito kwa chama cha mapinduzi na mwenyekiti wake ambae pia ndiye rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.


Kabla sijazungumzia ni kwanini mh. Kikwete afanye maamuzi mazito na magumu, nichukue nafasi hii kuwapongeza kipekee baadhi ya watanzania kwa nafasi zao:


1. kipekee nimpongeze mh. Anna Makinda kwa kuchaguliwa kwake kuwa spika wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kipindi cha 2010 – 2015. hongera sana. Nina uhakika hatawaangusha wanawake wa Tanzania kama sio Afrika nzima. Mh. Makinda amechaguliwa kuwa spika katika kipindi kigumu sana kwa mstakabali wa uhai wa taifa letu, kuna mawazo ambayo huamini kuwa mh. Makinda amepata uspika baada ya njia za kijasusi za kumdondosha spika aliyemtangulia. Na njama hizo za kijasusi zimefanyika na kupangwa na moja ya makundi yaliyosigana sana katika medani za siasa na ufisadi katika bunge lililopita. Kama mawazo haya yana ukweli japo kidogo, basi mh. Makinda ana kazi ngumu ya kujiondoa na kujinasua kwenye kundi hilo linalodhaniwa kupanga mipango hiyo ya kijasusi, kwani bila hivyo, watanzania na dunia yote inaweza kumtamfisiri mh. Makinda kuwa miongoni mwa kundi hilo kitu ambacho kinaweza kuhatarisha uhai wa bunge na mstakabali mzima wa taifa la Tanzania.






2. kipekee nimpongenze mh. Slaa aliyekuwa mgombea wa kiti cha uraisi kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) pamoja na chama chake kwa kuyakubali matokeo ya tume ya uchaguzi kama yalivyotangazwa na kuruhusu wabunge wake kuingia bungeni. Sina uhakika sana kama mh. Slaa kwa kukaa kimya kwake ni tafsiri ya “kubali yaishe ama anatunga sheria” katika hili siri yake anayo mwenyewe mh. Slaa na chama chake, lakini yatosha kumpongeza hata kwa hatua hii ya kufanya wabunge waapishwe kukiwa na usalama na utulivu. Hongera sana Dr. slaa na chama chako.






1






3. Mwisho kipekee nimpongeze mh. Samuel Sitta kwa kukubali yaliyomkuta, katika hili nisingependa kuongea mengi kwani siri ya mtungi aijuae kata, siri ya kuenguliwa kwake kwenye nafasi ya kugombea uspika kwa awamu ya pili kamati kuu ya CCM na mheshimiwa Sitta wanaijua wenyewe, iwe ni ujasusi ama demokrasia ndani ya chama cha mapinduzi ni siri yao wenyewe. Hata hivyo yatosha kumpa hongera mheshimiwa Sitta kwa hatua aliochukua ya kubali yaishe, kama wahenga wasemavyo wajenzi tusigombanie fito wakati nyumba tuijengayo ni moja na ni yetu sote.






Maamuzi mazito na magumu yanayostahili kuchukuliwa na mheshimiwa Kikwete pengine na bunge zima la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


1. kama imewezekana kwa maamuzi ya magumu na mazito yaliyofanywa na kamati kuu ya CCM kumpata spika mwanamke tena nje ya taratibu na kanuni za chama za kuongoza vipindi viwili kama ilivyo kwa mgombea urais, yawezakana kabisa pia waziri mkuu akateuliwa toka kambi ya upinzani. Nashauri hivi kwa sababu, siri ya matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi wanaoijua ni tume ya uchaguzi yenyewe, usalama wa taifa, pamoja na mh. Kikwete na Slaa na vyama vyao. Ninauhakika matokeo yaliyotangazwa CHADEMA na CCM wanajua undani wake kwani kila chama kina matokeo ya wagombea urais katika kila jimbo. Ni kwa msingi huu naomba hekima na busara zitumike kufikia maamuzi hayo magumu na mazito ya uteuzi wa waziri mkuu toka kambi ya upinzani, linalowezekana leo lisingoje kesho, tusingoje hadi damu imwagike kuleta mabadiliko hati miliki ya Tanzania ni ya watanzania wote.






2. Pili, kama Zanzibar imewezekana kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa Tanzania bara tunasubiri nini? Je tunasubiri watu waende shimoni? Tunasubiri damu imwagike? Tusisubiri kufika huko, serikali ya umoja wa kitaifa haina budi lazima iwe, hati miliki ya Tanzania ni kwa watanzania wote tena mikoa yote, katika historia ya Tanzania inaonekana uongozi wa juu wa serikali umemilkishwa kwa baadhi ya mikoa kama sio kikanda, hata mikoa iliyosahauliwa ni sehemu ya Tanzania na ni wamiliki wa Tanzania tusisubiri maafa yatokee. Tunashukuru Mungu marais wametoka kaskazini, mashariki, visiwani, na kusini ninaamini safari nyingine nyanda za juu kusini watakumbukwa kwenye nafasi hiyo nyeti. Lakini pia tumekuwa na mawaziri wakuu toka kaskazini, kanda ya kati, mashariki, na kusini na kiraka toka nyanda za juu, bado inaonekana nyanda za juu ni






2






wasindikizaji tu katika uongozi taifa hili la Tanzania. Tunahitaji serikali ya umoja wa kitaifa na kwamba Tanzania ni yetu sote, lazima tubadilike na wakati ni huu, mheshimiwa Kikwete afanye maamuzi magumu na mazito ili aje akumbukwe na mikoa iliyosahaulika.






3. Mwisho ni kwa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania, kama kwa matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi asilimia 39 ya wapiga kura imekubali mabadiliko ndani ya nchi, na narudia tena matokeo yaliyotangazwa ni ya kikatiba zaidi kuliko maamuzi ya wananchi, niwaombe waheshimiwa wabunge waache ushabiki wa vyama kwani wao ni wawakilishi wa watanzania, wafike mahali naibu spika atoke upinzani ili ile asilimia 39 ya watanzania iwakilishwe vyema kwenye maamuzi ya bunge na hapo tutakuwa tunajenga umoja wa kitaifa. Pia tuzingatie kuwa matokeo yaliyotangazwa na idadi ya wapiga kura waliopiga kura ni asimia 27 tu ya watanzania wenye sifa na stahiki ya kikatiba ya kupiga kura, maana yake hata viongozi waliotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi wametangazwa kimakosa, kwani wamechaguliwa na watanzania wenye haki ya kupiga kura chini ya nusu, kuna haja ya kulitazama zaidi suala hili, tupate bunge lenye sura ya umoja wa kitaifa na uwakilishi sawa kwa watanzania wote.






Imetolewa na: Kimbombo Andrew Uswege TAREHE 14/11/2010


Chuo Kikuu Mkwawa – Iringa


Simu: 0754/0715/0786 - 261870

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...