Skip to main content

MADIWANI SIMAMIENI UTUNZAJI MAZINGIRA- DR. HOVISA

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – (Mazingira) Dr. Terezya Luoga Hovisa amewataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma kusimamia kwa karibu sana masaula ya utunzaji mazingira katika kata zao zote, kwa kuwa uharibufu wa mazingira ni tatizo la dunia nzima na kuongeza kuwa tunakoelekea ni kubaya zaidi kwa kuwa madhara ya uharibifu wa mazingira yanaonekana zaidi katika jamii.


Hayo yalisemwa na waziri wa mazingira huyo alipokuwa akizungumza na madiwani walipokuwa katika kikao cha kamati cha madiwani kilichofanyika Songea mjini katika Ukumbi wa Tumbaku (NGOMATI).


Waziri huyo alisema kwamba atahakikisha na atasimamia kwa nguvu na juhudi zake zote suala la uharibifu wa mazingira na hivyo madiwani wahamasishe wananchi katika maeneo yao wanakotoka. Aliwataka madiwani hao kuwashauri wananchi wao ambayo sehemu kubwa ni wakulima wadogo wadogo kwamba tabia ya kukata miti yote katika mashamba yao wakati wa kulima na kufanya palizi basi watunze miti kadhaa katika mashamba yao.


Dr. Hovisa alidokeza kwamba wameanza na anaendelea kuwashawishi wahisani mbalimabli kusaidia katika upatikanaji wa nishati mbadala (alternative source of energy), kwa kuwa tatizo la nishati ndiyo chanzo kikubwa cha uharibufu wa mazingira.


Waziri huyo alifika Songea kufuatia taarifa aliyopewa kwamba tarehe 15/12/2010 ingekuwa ni siku ya kuaapishwa kwa madiwani na kuzinduliwa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Songea na badala yake siku ya kuaapishwa kwa madiwani itafanyika kesho Ijumaa.


Wakati huo huo, Chama cha Mapinduzi (CCM) Halmashauri ya Songea vijijni wamemchagua Bw. Rajabu Hassani Mtiula diwani wa Kata ya Mpitimbi kuwa mwenyekiti wa halmashauri katika uchaguzi wa kura za maoni uliyofanyika jana. Bw. Mtiula alipata kura 19 dhidi ya mpinzani wake Bw. Jumanne Alex Nyingo diwani wa Kata ya Litisha aliyepata kura tatu tu.


Msimamizi wa uchaguzi Bi. Lidya Gunda Jonh ambaye pia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Vijijini alisema kuwa idadi ya waliopiga kura ilikuwa ni 22 ambapo walikuwa ni madiwani wa kata, madiwani viti maalumu pamoja Mhe. Mbunge Jenister Mhagama (MB Peramiho).


Alisema kuwa kura zilikuwa za siri kubwa kwani walitumia karatasi maalum na kuongeza kuwa wagombea wa nafasi ya mwenyekiti walikuwa wagombea wawili tu waliojitokeza.


Kwa upande wa makamu mwenyekiti, msimamizi wa uchaguzi alimtangaza Bw. Theofani Tadei Mbelwa kuwa makamu mwenyekiti baada ya kupata kura 20 za ndiyo katika kinyang’anyiro ambapo mwenzake alijitoa dakika ya mwisho na kumuunga mkono mwenzake kwa kuwa alikuwa na hoja ya msingi kuliko yeye.


Wakipewa nafasi ya kushukuru wagombea hao kwa pamoja walisema kuwa madiwani wanapaswa kuvunja makundi katika baraza la madiwani na badala yake kujenga umoja na mshikamano na kuachana na sera za kujenga mpasuko katika baraza hilo la Halmashauri ya Songea (W).


Halmashauri ya Wilaya ya Songea vijijni ina jumla ya madiwani 24 wakiwemo madiwani wawili kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...