Skip to main content

MBEGA ANG'OWA MAPAZIA NA SAMANI OFISI YA MBUNGE

Tumaini Msowoya,
Iringa


VITENDO vya wabunge wa CCM kuhamisha samani na vitu vingine kwenye ofisi za wabunge majimboni, jana liliibukia Iringa Mjini ambako mbunge mpya kwa tiketi ya Chadema, Peter Msigwa amedai kuikuta ofisi ikiwa imeondolewa kila kitu, ikiwa ni pamoja na kung'olewa kwa mapazia.

Msigwa anadai kuwa vitu hivyo vimeondolewa na mbunge aliyemaliza muda wake, Monica Mbega, ambaye alianguka vibaya kwenye uchaguzi wa mwaka huu baada ya kuliongoza jimbo hilo kwa miaka kumi.


Kitendo hicho kimeibuliwa siku chache baada ya taarifa za kuondolewa thamani na vitasa kwenye ofisi ya mbunge wa Jimbo la Nyamagana. Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha ndiye aliyeng'oa samani hizo baada ya kushindwa na mgombea wa Chadema, Ezekiel Wenje.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake jana, Msigwa ambaye alianza kazi Jumatatu, alidai aliikuta ofisi hiyo ikiwa katika hali ya uchafu huku ikiwa haina mapazia, kompyuta, simu, nyaraka wala faili za kuhifadhia taarifa muhimu licha ya kuwa ilikuwa ikitumika katika kipindi kilichopita.

Alisema kuwa kutokana hali ya uchafu, alilazimika kupaka rangi ofisi hiyo iliyo katika jengo la
Halmshauri ya Manispaa ya Iringa na kisha kufunga simu mpya baada ya ile iliyokuwepo kuonekana imenyofolewa.

“Ofisi nimeikuta katika hali ya uchafu sana; haina simu wala nyaraka yoyote inayoonyesha kama ofisi hii ilikuwa ikifanya kazi katika kipindi kilichopita. Hali hii ni hatari ikiwa kweli, viongozi tuna nia ya kuwatumikia wananchi,” alisema Mchungaji Msigwa.

Alisema kuwa hakuna makabidhiano mazuri ambayo yamefanyika katika ofisi hiyo na kwamba amelazimika kuanza na kutengeneza vitasa ambavyo vilikuwa vimeharibika, ili kuhakikisha ofisi hiyo inakuwa katika hali ya usalama.


Alisema alipotaka kujua sababu ya ofisi kuwa katika hali hiyo, alidai kujibiwa kuwa vifaa vilivyokuwemo vilinunuliwa na Monica Mbega na kwamba kwa kuwa amemaliza muda wake, amelazimika kuondoka na kila kitu ambacho alinunua kwa ajili ya kulitumikia jimbo hilo.

“Nimeuliza kwa nini ofisi hii haina kitendea kazi wala nyaraka yoyote inayoonyesha kwamba ilikuwa ikifanya kazi, jibu nililopewa ni kwamba Mama Mbega andiye aliyenunua hivyo kwa hiyo ni vitu vyake na ameamua kuondoka navyo,” alisema.


Alipopigiwa simu na Mwananchi ili azungumei madai hayo, Mbega alikata simu mara baada ya mwandishi kujitambulisha kuwa anatoka gazeti hili.
Pia simu hiyo iliendelea kukatwa pale mbunge huyo wa zamani alipopigiwa mara ya pili na ya tatu na baada ya hapo ilikuwa ikiita bila majibu.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo alisema licha ya kwamba ofisi hiyo ipo kwenye jengo la halmashauri hiyo, inahudumiwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya.


Hata hivyo, katibu tawala wa Wilaya ya Iringa, Gidion Mwinami alisema ofisi yake haijawahi kufanya tathmini kujua ndani ya ofisi hiyo kulikuwa na nini hivyo ikiwa kweli, Mbega alinunua vifaa hivyo, ana haki ya kuondoka navyo.


“Sifahamu kulikuwa na nini, na sisi hapa hatujaletewa oda kwamba ofisi ya mbunge inahitaji kuwa na nini. Kama kweli vifaa vilivyokuwepo alinunu mbunge aliyepita, ni haki yake,” alisema.


Alisema kuwa anachofahamu yeye ni kwamba ofisi hiyo ya mbunge inapaswa kuhudumiwa na serikali na kwamba meza moja sambamba na makochi ndivyo vilivyokuwepo, lakini hajui kama kulikuwa na kitu kingine zaidi ya hivyo.


“Kulalamika ni hulka ya mtu, nyie mmefika na kuona kuwa hapo kuna upungufu wa kitu gani; kama pazia pisi ngapi hazipo? Sisi hatujafanya tathmini kubaini hili ila tutafanya hivo,” alisema
Msigwa alisema kutokana na ukweli kwamba, uongozi wa jimbo ni wa kupokezana kwa kuzingatia ridhaa ya wananchi, ni vyema mbunge anayekuwa madarakani akajitahidi kuhifadhi nyaraka ili mbunge anayeanza ajue kilichofanyika, na wananchi gani walihudumiwa tofauti na hali ilivyo katika ofisi hiyo.


Hata hivyo, alisema kuwa yupo katika mchakato wa awali wa kuajiri mwanasheria kwa ajili ya kusikiliza matatizo ya wananchi wanaohitaji msaada wa kisheria ambao wamekuwa wakikosa haki zao kwa kutojua sheria.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...