Skip to main content

ZAWADI YA MKESHA WA NOELI

Muuguzi wa Zamu wa St. Joseph's Mission Hospital Peramiho akiwa anawaangalia watoto ambao walizaliwa kabla ya umri yaani 'Premature babies' katika Chumba cha Joto 'Premature Unit or Incubator Room' Jumamosi kuangalia kama wanaendelea vizuri lakini hawakuzaliwa kwenye Mkesha wa Krismasi wako wanne.

Baadhi ya kina mama waliojifungua wakiwa wamepakata watoto wao katika Mkesha wa Krismasi katika  Hospitali ya Mtakatifu Joseph Peramiho Songea Vijijini, Mkoa wa Ruvuma.


Na Friday Simbaya,



Peramiho


JUMLA ya watoto 13 wamezaliwa, wakiwemo wakike tisa na wakiume wanne katika Hospitali ya Mission ya Mtakatifu Joseph Peramiho mkoani Ruvuma katika Mkesha wa Noeli (Krismasi) usiku wa kuamkia LEO.


Akiongea na BLOG HII, Muuguzi wa Zamu (Nursing Office in charge), Bi. Sirah Nchimbi alisema kwamba watoto wote walizaliwa kwa njia ya kawaida isipokuwa watoto watatu ndiyo waliozaliwa kwa njia ya upasuaji (surgical operation) lakini hali zao zinaendelea vizuri pamoja na mama zao.


“Watoto hao walizaliwa na uzito wa kawaida, hali zao zinaendelea vizuri sana pamoja mama zao. Wakina mama wengine wameruhusiwa baada ya kujifungua lakini wamebaki wale walioji fungua kwa opresheni ambao wako katika uangalizi maalumu,” alisema muunguzi wa zamu.


Aidha, alisema kuwa yapo matatizo wanayokubiliana nayo kama vile kina mama kutofika mapema hospitalini pindi wapatapo uchungu wa uzazi kunako sababisha wengi wao kinamama kujifungulia njiani kabla ya kufika hosptali na wengi wao hujifungua watoto waliokufa katokana na kuchelewa kufika hospitali mapema.


Tatizo jingine ni kwamba wa kinamama walio wengi maeneo haya hutumia dawa ya mitishamba kuongeza uchungu wa kujifungua kabla ya kuletwa hospitali, matokeo yake wengi wao kina mama wanashindwa kujifungua kwa njia ya kawaida (normal delivery) au hujifungua watoto waliokufa kutokana na dawa hizo wanazozitumia.


“Yaani ni tatizo kubwa sana kwa kina mama wanaokuja kujifungua hapa kutokana kutumia dawa za kienyeji za uchungu lakini huwatunawapa elimu wanapofika na kuwapa ushauri wakina mama wajawazito waweze kufika hospitalini mapema na kuacha kutumia dawa hizo za kuongeza uchungu, ambapo mara nyingi hutiwa kwenye chain a uji,” alisema muunguzi huyo wa zamu.


Lakini pamoja na hayo, hakuweza kuelezea ni dawa ya aina gani mara nyingi wa kina mama hao hutumia kama dawa ya kuongeza uchungu, na kuongeza kuwa wanatumia mizizi Fulani Fulani ambayo hakutaja aina gani ya mizizi hiyo.


Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...