Skip to main content

JKT RUVU YABAMIZA MAJIMAJI 1-0

Na Friday Simbaya,



Songea






TIMU ya Soka ya Majimaji ya Songea jana ilishindwa kutamba mbele ya JKT Ruvu ya Dar es Salaam baada ya kufungwa bao 1-0 mbele ya mashabiki wake katika Ligi Kuu Soka Bara mzunguko wa pili.






Ruvu ambayo walicheza vizuri na kutumia makosa ya mabeki wa Majimaji ilipata bao lake la kuongoza katika dakika 15 ya kipindi cha kwanza.






Majimaji walipata pigo baada ya beki wa kati Mudi Mupopo kutolewa nje baada ya kupatikana na kadi za njano mbili na kufanya timu hiyo kucheza pungufu.






Timu hiyo ya Majimaji ilitokea nchini Msumbiji waliko kwenda kucheza mechi za kirafiki na timu mbalimbali za nchini humo kwa ajili ya kujiweka tayari kwa ajili ligi kuu Bara mzunguko wa pili.






Wakitokea nchini Msumbiji ambapo walishinda baadhi ya mechi walipiga kambi kama ‘stop over’ Peramiho Songea Vijijni kabla ya kucheza na Tium ya JKT Ruvu katika Uwanja wa Majimaji Mjini Songea Mkoani Ruvuma jana.






Akizungumza na Nipashe baada ya kumalizika kwa mpira, beki wa Majimaji Evarist Maganga alisema hawakuwa na bahati licha ya kucheza nyumbani jana kutokana na kufungwa na Timu JKT Ruvu pamoja na kuwa na maandalizi ya kutosha.






Aliongeza kuwa wakazi wa Ruvuma wasife moyo kutokana na kufanya vibaya katika mechi katika Ruvu na Majimaji kwa sababu mambo mazuri yanakuja mbeleni na kuwaomba waendelee kuipa sapoti ya kutosha.






Kocha Mkuu wa timu ya Majimaji, Sebsatian Mkoma, aliwataka wakazi wa Ruvuma kuipa sapoti timu yao Majimaji ili ifufuwe matumaini ya kusonga mbele. Hata hivyo, wakazi wa Ruvuma hawakujitokeza kwa wengi kama ilivyotegemewa na timu hiyo ya wanalizombe






Nkoma ambaye amepewa majukumu ya kuliokoa jahazi hilo la Majiamaji ambalo linaonkana kuzama, alisema bado timu hiyo inanafasi ya kufanya vizuri na kubaki katika ligi kuu msimu huu.






Alisema kuwa ziara ya majimaji nchini msumbiji ilikuwa ni sehemu ya maadalizi ya kujiweka vyema kwa ajili ya ligi kuu soka bara mzunguko wa pili.






Hata hivyo, Timu ya Majimaji itamenyana na Timu ya African Lyon tarehe 20 Januari, 2011 Mjini Morogoro.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...